Sunday, August 12, 2018

MKURUGENZI MTENDAJI CRDB BANK, DK. KIMEI ATEMBELEA OFISI ZA MKOA ZA SIDO JIJINI DAR ES SALAAM, AZUNGUMZA NA WANASEMINA WAJASIRIAMALI


Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (kushoto), akiwa pamoja na mwenyeji wake, Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga, wakiwasili katika ukumbi wa semina ya wajasiriamali wa Sido, walipofika kwa ajili ya kuzungumza nao, mwishoni mwa wiki Vingunguti jijini Dar es Salaam.   
Wanasemina wajasiriamali wa Sido, wakimpokea Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (hayupo pichani), wakati alipowatembelea na kuzungumza nao katika mafunzo yao ya wiki moja, Sido mkoani wa Dar es Salaam. 
Baadhi ya Maofisa wa CRDB Bank, walioambatana na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dk. Charles Kimei, wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na mkurugenzi huyo, kwenye mafunzo ya wajasiriamali wa Sido, Mkoa wa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Mwandamizi Dawati la Akinamama, Rehema Shambwe, Meneja Mwandamizi Wateja Biashara Ndogo na za Kati, Mussa Mwinyidaho (katikati) na kulia ni Meneja Uhusiano wa CRDB, Rachel Senni.
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, akizungumza na wajasiriamali wa Sido, wakati wa semina yao, iliyofanyika Sido Mkoani, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kulia ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga, Ofisa Mtendaja Mkuu wa Kampuni ya Mlako Purified Ice Cubes, Joseph Mlay (kushoto) na Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka.
Baadhi ya wanasemina wajasiriamali, wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei, wakati alipowatembelea na kuzungumza nao katika mafunzo yao ya wiki moja, Sido Mkoani Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
Baadhi ya wanasemina wajasiriamali, wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei.
Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga, akizungumza wakati akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (kushoto). 
Mwenyekiti wa semina ya wajasiraimali wa Sido, akitoa shukurani kwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei. 
Meneja wa Kampuni ya kutengeneza manukato na vipodozi ya efa, Obed Musiba (kulia), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia), kuhusu chupa za vipodozi na manukato zinazotengenezwa na moja ya mashine zao kwenye kiwanda chao. Kushoto ni Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga.
Meneja wa Sido Mkoa wa Dar es Salaam, MacDonald Maganga (katikati), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (kulia), kuhusu mashine ya kutengenezea chupa za vipodozi na manukato (kushoto), alipotembelea sehemu za uzalishaji Ofisi za Sido Mkoa wa Dar es Salaam katika ziara hiyo. 
Fundi mitambo wa Kampuni ya PEC, Hans Mzalia (kulia), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (wa pili kulia), kuhusu mashine ya kuzalisha umeme kwa maji zinazotengenezwa na kampuni hiyo. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Sido Incubator Programme Star Natural Products, George Buchafwe (kulia), amkimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (katikati), kuhusu vipuri vya mashine za kutengenezea sabuni vinavyotengenezwa na kampuni yake katika Ofisi za Sido Mkoa wa Dar es Salaam, jijini. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka.   
Mkurugenzi wa Kampuni ya Sido Incubator Programme Star Natural Products, George Buchafwe (kulia), amkimuonesha Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (katikati), baadhi ya malighafi zinazotumika kutengenezea sabuni kwenye kiwanda chake, ofisini hapo. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa benki hiyo, Jessica Makhuka.  
Meneja Mwendeshaji wa Kampuni ya kuzalisha asali ya Miyombo Golden Resource, Kundaeli Urassa (kulia), akimpatia maelezo Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank, Dk. Charles Kimei (kushoto), kuhusu asali inayozalishwa na kampuni hiyo.

No comments: