Tuesday, June 26, 2018

DOKTA PHILIP MPANGO AHITIMISHA MJADALA WA BAJETI BUNGENI JIJINI DODOMA

  Baadhi ya wadau wakifuatilia kwa makini mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, kabla ya Waziri mtoa hoja Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) hajahitimisha hoja hiyo ya Bajeti, Bungeni, Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Adelardus Kilangi, wakizungumza jambo kabla ya kuhitimishwa kwa hoja ya mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni Dodoma.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na Naibu wake Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), wakifuatilia hoja za Mawaziri wakati wa kuhitimisha hoja ya mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni, Dodoma.

 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), akijibu hoja mbalimbali za wabunge wakati wa kuhitimishwa kwa hoja ya mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni Dodoma, ambapo alizitaka Halmashauri kuendelea kubuni miradi ya kimkakati ili kujiongezea kipato.

 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akihitimisha hoja ya mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni, Dodoma, ambapo ameahidi kusimamia mapato na matumizi ya fedha za umma kwa ufanisi na kuwatahadharisha wabadhilifu wa fedha za umma kuwa ni sawa na kula sumu. 
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), na Waziri wa Madini, Mhe. Anjellah Kairuki (Mb), wakijadili jambo muda mfupi baada ya kuhitimishwa kwamjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni Dodoma.

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatib Kazungu (katikati), akipeana mkono na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhandisi Gerson Lwenge, katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma baada ya kuhitimishwa kwa hoza za Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka 2018/19, ambapo mtoa hoja  Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani) aliwapongeza wabunge wengi kwa kutoa hoja zenye kujenga ili kuboresha Bajeti hiyo, kulia ni Kamishna Msaidizi wa Sera wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Shogholo Msangi. 
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto), akipongezwa na Mbunge wa Kiembe Samaki Mhe. Ibrahim Raza kwa hitimisho zuri la Hoja ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa kusisitiza weledi katika usimamizi wa fedha za umma.

 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akipongezwa na Mbunge wa Kwimba Mhe. Mansoor Sharif, baada ya kuhitimisha ya Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mipango madhubuti ya kufikia uchumi wa kati. 
NaibuWaziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) akipongezwa na Mhe. George Simbachawene (Mb) (kushoto) na Waziri wa Habari,  Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, kwa kujibu hoja za wabunge kwa ufasaha wakati wa kuhitimisha mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali kwa Mwaka 2018/19, Bungeni, Dodoma.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikali-Wizara ya Fedha na Mipango)

No comments: