Thursday, May 10, 2018

Waziri Dkt. Mahiga afanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi wa Israel

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akipeana mkono na Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman walipokutana jijini Tel Aviv leo asubuhi kwa ajili ya kufanya mazungumzo 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga na ujumbe wake (kulia) na Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo ambapo walijadili masuala mbalimbali ikiwemo kushirikiana katika masuala ya ulinzi na usalama. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga wa kwanza kulia na akifuatiwa na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima na Afisa Dawati wa Israel, Bi Kisa Mwaseba wakiwa katika mazungumzo na ujumbe wa Israel. 
Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman wa kwanza kulia akisisitiza jambo kwenye mazungumzo hayo. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akikabidhi zawadi kwa Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman walipokutana jijini Tel Aviv leo asubuhi. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga naye akipokea zawadi kutoka kwa Waziri wa Ulinzi wa Israel, Mhe. Avigdor Liberman jijini Tel Aviv leo asubuhi. 
Kaimu Mkurugenzi wa Mashariki ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Suleiman Salehe akisalimiana na Waziri wa Ulinzi wa Israaele, Mhe. Avigdor Liberman. 
Waheshimiwa Mawaziri wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Israel, Mhe. Job Masima wa kwanza kushoto na Balozi wa Israel nchini Kenya ambaye anawakilisha pia Tanzania. 

No comments: