Saturday, May 5, 2018

MBEYA PRESS CLUB WAADHIMISHA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI KWA MJADALA MKUBWA KATIKA UKUMBI WA MKAPA JIJINI MBEYA

Mkuu wa wilaya ya Mbeya Bw. Paul Ntinika akizungumza wakati akifungua mkutano wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya (Mbeya Press Club) unaofanyika leo kwenye ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ambayo yanafanyika kila mwaka Mei 3 waadishi wa Habari mkoa wa Mbeya wamadhimisha siku hiyo leo, Kutoka kulia ni Frank Leonard Mwenyekiti wa Press Club Iringa, Modest Nkurlu Mwenyekiti wa Mbeya Press Club na kushoto ni Fredy Jackson Kaimu Katibu Mkuu Mbeya Press Club. KAULI MBIU ya maadhimisho hayo mkoa wa Mbeya ni "Uhuru wa Vyombo vya habari ni Chachu ya Uwajibikaji kwa Maendeleo ya Mkoa wa Mbeya" 
Mkuu wa wilaya ya Mbeya Bw. Paul Ntinika wa pili kutoka kushoto akimsikiliza Frank Leonard Mwenyekiti wa Iringa Press Club wakati akizungumza katika mkutano huo kama mmoja wa wageni waalikwa, katikati ni Modest Nkurlu Mwenyekiti wa Mbeya Press Club na kushoto ni Fredy Jackson Kaimu Katibu Mkuu Mbeya Press Club.
Frank Leonard Mwenyekiti wa Iringa Press Club akichangia mada katika mkutano huo.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Mbeya Bi. Julieth Godrey Manech akichangia na kutoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali kwa upande wa Taaisis ya Kuzuia rushwa nchini TAKUKURU jinsi waandishiwa wanavyoweza kushirikiana na tasisi hiyo
Mwanahabari Charles Mwakipesile pamoja na baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya.
Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mjadala huo.
Mdau Joseph Mwaisango ni mmoja wa wanahabari walioshiriki katika maadhimisho hayo.
Wadau mbalimbali wakiwa wakifuatilia majadiliano katika mkutano huo
Mwanahabari Naomi Malala akizungumza jambo na mwanahabari mwenzie Rachel Mwangosi huku Plaxeda Mbullu akiwasikiliza.
  
Keneth Simbaya Rais Mstaafu wa Vyama vya waandishi wa habari nchini UPC pamoja na washiriki wengine wakiwa katika mkutano huo.
Mkuu wa wilaya ya Mbeya Bw. Paul Ntinika akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari mara baada ya kufungua mkutano wa Chama cha waandishi wa habari mkoa wa Mbeya (Mbeya Press Club) unaofanyika leo kwenye ukumbi wa Mkapa jijini Mbeya ikiwa ni maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ambayo yanafanyika kila mwaka Mei 3

No comments: