Saturday, April 28, 2018

Watoto wawili kuiwakilisha Tanzania kombe la Dunia Russia 2018

Programu ya Football for Friendship (F4F) 2018 inabadilisha ndoto ya kombe la Dunia la FIFA kuwa kweli kwa Zipora Mollel pamoja na Laigwanani Lomayani Mollel, vijana hao kutoka kabila la Maasai wamechaguliwa kwenda Russia kuiwakilisha Tanzania huku gharama zote zikibebwa na F4F. 

F4F ni programu ya kimataifa ya watoto ya kila mwaka inayoratibiwa na kampuni ya kimataifa Gazprom ambayo inaunga mkono miradi ya kijamii ulimwenguni na kuweka viwango vipya kuhusiana na sera za kijamii.

Inatarajiwa kufanyika Moscow, Russia kuanzia Juni 8-15, kuelekea michuano ya Kombe la Dunia, lengo la programu hii ni kutangaza maadili yanayohusiana na mpira wa miguu kwa vijana wadogo ikiwa ni pamoja na kuheshimu mila, utaifa na usawa.

Laigwanani Mollel ataiwakilisha Tanzania akiwa mchezaji anayechipukia wakati Ziporah Mollel yeye atashiriki kama mwanahabari chipukizi, watakuwa wawakilishi wa nchi kwenye kombe la Dunia licha kwamba timu ya taifa imeshindwa kufuzu katika mashindano hayo. Wataungana na wachezaji wenye umri wa miaka 12 pamoja na waandishi kutoka mataifa 210 na kujumuika kushiriki programu ya siku nane (8).

Mwaka 2018 mataifa mapya 147 na kanda zitashiriki programu ya F4F inayohusisha watu 3,700 wenye umri kati ya miaka 12 na 16 walioshiriki program hiyo kwa zaidi ya miaka mitano.

Laigwanani Mollel na Ziporah (miaka 12) wataambana na meneja wa uendeshaji kutoka Lengo Football Academy, Bw. Amani Mzava, kocha Bw. Alvin Girelisu. Lengo Football Academy inajivunia kushirikiana na Clouds FM na Clouds TV. Mwanahabari mashuhuri wa michezo Shaffih Dauda kutoka Clouds FM/TV ataongozana na msafara wa watanzania kwenda Russia kuiwakilisha Tanzania.

Jumla ya timu 32 za kirafiki za kimataifa zitashindana katika mechi za kirafiki kucheza mpira wa miguu 'Friendship World Championship' Juni 12, 2018. Kuelekea mashindano hayo  kila mchezaji atafundishwa makocha watoto ambao ambao ni wachezaji wenye umri kati ya miaka 14 na 16 kutoka mataifa tofauti. 

Zaidi ya vyombo vya habari 5,000 kutoka sehemu mbalimbali Duniani vitaripoti progamu  hiyo kitu ambacho kinatazamiwa na Umoja wa Mataifa kuwa ni elimu ya kipekee. Vyombo vya habari vitashirikisha waandishi wa habari watoto wa F4F wenye umri wa miaka 12 kutoka nchi 211 wataripoti habari zao za F4F ambazo zitasambaa ulimwengu mzima.

Fursa hii ni matokeo ya F4F (RUS) programu inayoendelea kwa kushirikiana na Lengo Football Academy (TZ) ambayo imeidhinishwa na TFF. Lengo Football Academy ni shirika la Tanzania na Australia linalosaidia vijana wa Arusha, Tanzania kwa kutumia nguvu ya mpira wa miguu kutengeneza njia kwa vijana kufikia ndoto zao kwenye maisha ndani na nje ya uwanja. Lengo Football Academy inashirikiana na Football for Friendship (F4F) kusaidia nchi 12 kuhudhuria programu ikijumuisha Tanzania, Australia, New Zealand pamoja na nchi 9 za visiwa vya Pasific.

Emanuel Saakai, mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Lengo Football Academy amesema, "tunafurahi kushirikiana na Football for Friendship na kupata fursa ya kutoa vijana wawili kutoka kwenye Academy yetu ya Arusha kwenda kupata uzoefu. Tumepata upendeleo kuandaa programu hii kwa nchi nyingi Duniani kote, hakika tutaiweka Tanzania kwenye ramani ya Russia 2018.

No comments: