Tuesday, April 10, 2018

MAKAMU WA RAIS AZINDUA CHANJO YA KUKINGA SARATANI YA KIZAZI JIJINI DAR ES SALAAM




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa ameshikilia chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem, wengine pichani ni mabinti waliokuwa wa kwanza kupatiwa chanjo hiyo wakati wa uzinduzi, kushoto ni Neema Felix (14) mkazi wa Mbagala na mwingine ni Hadija Bakari (14) mkazi wa Kigamboni.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu (katikati), Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu pamoja na wadau wengine wa Afya wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa tuoaji wa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) uliofanyika kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem, jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishuhudia Binti mwenye umri wa miaka 14 anayefahamiaka kwa jina Hadija Bakari mkazi wa Kigamboni akichomwa chanjo ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) wakati wa uzinduzi wa chanjo hiyo kwenye viwanja vya Mbagala Zakhem wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na mabinti wa kwanza kupata chanjo ya ya kukinga saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine), aliyesimama kushoto ni Hadija Bakari (14) mkazi wa Kigamboni na kulia ni Neema Felix (14) mkazi wa Mbagala.

No comments: