Saturday, February 10, 2018

WATENDAJI TIMIZENI WAJIBU WENU KUONDOA MIGOGORO – IYOMBE

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe amewaasa watendajii wa mkoa wa Manyara kuchukua hatua stahiki zinazohusu masuala ya watumishi ili kupunguza au kuondoa migogoro mkoani Manyara.

Katibu Mkuu Mhandisi Iyombe ameyasema hayo mjini Babati wakati akiongea na watendaji na watumishi wa Mkoa wa Manyara, Halmashauri ya Mji Babati na Halmashauri ya Wilaya Babati kwamba kiwango kikubwa cha migogoro hasa ya ardhi mkoani humo inatokana na baadhi ya watendaji kutotimiza wajibu wao ipasavyo hali wakizingatia sheria na taratibu za nchi.

“migogoro mingi inaanzia Sight (sehemu wanazotwaa ardhi ili kupima) kwa kuleta taarifa iliyo na mapungufu na pia zingatieni sheria za ardhi, migogoro ipungue kwa kwa kutenda”
Pia Mhandisi Iyombe amesema wapo Watendaji ambao wanashindwa kutumia Mamlaka waliyopewa na kuzuia migogoro ya ardhi ambayo inazuilika lakini pia amehoji mbona mipaka ya mikoa na wilaya ipo wazi na kwanini sehemu nyingine za kiutawala, “msilazimishe migogoro ya ardhi kwani tumewapa mamlaka kwa kufanya Ugatuaji wa madaraka (D by D) hivyo amueni”

Akipokea taarifa ya elimu kuhusu kuwashusha vyeo walimu wakuu zaidi ya 250, ametoa angalizo kuwa mamlaka na Uongozi wa mkoa mzima unapaswa kushauriana katika masuala mbalimbali kama hilo la elimu kabla ya kuchukua maamuzi magumu ambayo hayajafanyiwa utafiti wa kina kwani yanaleta athari kiutendaji na kisaikolojia kwa watumishi. Mhandisi Iyombe amewataka watendaji wa mkoa kuepuka suala la kuwa na Maafisa wengi wanaokaimu hali sheria zipo wazi kwani kufanya hivyo kunapunguza hamasa ya utendaji na kuongeza gharama zisizo za lazima. 

“suala la kukaimu lisizidi miezi sita ili kuboresha utendaji, kwanini Halmashauri zingine wanakaimu hadi miaka mitatu” amewataka kufuata sheria za kazi ili kupunguza hoja zisizo na msingi.Kwa upande wake Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Misaile Mussa amesema mkoa wa manyara una upungufu wa watumishi wapatao 6644 kwa mkoa mzima ambapo watumishi 2,076 wapo Halmashauri ya wilaya ya Babati. 

Lakini pia mkoa unakabiliwa na Maafisa wengi wanaokaimu kuanzia ngazi ya mkoa na Halmashauri za mkoa huo.Naye Mkuu wa wilaya ya Babati, Mhe.Raymond Mushi amesema kuwa changamoto ya upatikanaji wa maji na hasa ya miundombinu ya kupeleka maji na pia mipaka ya wilaya ya Babati na Monduli, na Babati na Kondoa anaendelea kufuatilia kuona mipaka halisi mahali ilipo.

Katibu Mkuu Mhandisi Mussa Iyombe yupo katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Manyara ambapo leo hii ameongea na watumishi hali akisikiliza kero zao na kuzitolea majibu papo hapo na kesho atatembelea miradi ya maendeleo kujionea jinsi inavyotekelezwa
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Babati na Babati Mji katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Babati wakati wa ziara yake leo
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe akiongea na watumishi wa Halmashauri ya Babati na Babati Mji katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya Babati wakati wa ziara yake leo
Baadhi ya Wakurugenzi wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) walioshiriki ziara ya Katibu Mkuu OR TAMISEMI Mha. Mussa Iyombe wakiwa katika chumba cha mikutano Babati leo
Katika picha ya pamoja ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara Misaile Mussa wakisikiliza taarifa ya Halmashauri ya Mji Babati
Baadhi ya watumishi wa ofisi ya Mkoa wa Manyara, Babati Mji na Halmashauri ya Wilaya Babati wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe alipokuwa akiongea nao mjini Babati leo
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhandisi Mussa Iyombe alipowasili katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Babati kuongea na watumishi leo

No comments: