Thursday, February 1, 2018

UONGOZI WA CCM MKOA WA PWANI WALAANI VIKALI VITENDO VYA WATU WANAOHUJUMU ZAO LA KOROSHO

Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa chama kikuu cha ushirika (CORECU) hawapo pichani baada ya kufanya ziara katika ofisi zao kupata taarifa ya baadhi ya watu wanaohujumu zao la korosho.
Mwenyekiti wa chama kikuu vha ushirikika Mkoa wa Pwani (COORECU) Rajab Ng’onoma akitoa ufafanuzi kwa viongozi wa CCM Mkoa wa Pwani kuhusiana na mwenendo mzima wa zao la korosho pamoja na changamoto amabzo zinawakabili katika utendaji wao wa kazi.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya CORECU wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani mara baada ya kumalizika kwa kutano wa kujadili masuala mbali mbali ya zoa la korosho.PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU




VICTOR MASANGU-PWANI

SAKATA la kuhujumu zao la korosho linalofanywa na baadhi ya wanunuzi,wakulima,pamoja na viongozi wa vyama vya ushirika hatimaye limechukua sura mpya baada ya uongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kuamua kuliingilia kati suala hilo kwa lengo la kuweza kuwabaini wale wote ambao wanahusika kwa namna moja au nyingine ili waweze kuchukulia hatua kali za kisheria.

Uamuzi huo wa CCM mkoa wa Pwani umekuja kufuatia kuwepo kwa taarifa ya kuibuka vikundi vya watu wachache ambao wana lengo la kukwamisha juhudi za serikali ya awamu ya tano kutokana na kuamua kufanya vitendo vya kuhujumu zao hilo kwa kuweka mawe,michanga, na takataka katika magunia ya korosho kitu ambacho ni kinyume kabisa na sheria na taratibu za nchi.

Akizungumza katika ziara ya kushitukiza katika ofisi za Chama kikuu cha ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) kwa ajili ya kupata ufafanuzi juu ya jambo hilo Mwenyekiti mpya wa CCM Mkoa Ramadhani Maneno alisema kuwa suala hilo limemchukiza sana hivyo hawezi kulifumbia macho na atalivalia njuga kwa lengo la kuweza kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli ya kupambana na watu ambao ni wezi na mafisadi.

“Sisi kama chama cha CCM mkoa wa Pwani tumeamua kuja hapa kwa ajili ya kupata maelekezo juu ya suala hili la baadhi ya watu ambao wanahujumu zao la korosho kwa kweli na kwa kuwa tunatelekeza ilani ya chama kwa kweli hatuwezi kulivumilia tutahakikisha tunashirikiana na vyombo vya dola katika kulifanyia kazi suala hili la kuwapata wale ambao wanajihusisha,”alisema Maneno.

Naye mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) kutokea Mkoa wa Pwani Haji Jumaa alisema kuwa lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatekeleza ilani ya chama ipasavyo ili kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi wote hususan kuweza kuwatetea wakulima waweze kupata haki zao za msingi wanazostahili bila ya kuzulumiwa na watu wachache.

Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) Rajab Ng’onoma amesema wamekuwa wanakabiliwa na changamoto ya kushuka kwa ubora wa korosho ambao umesababishwa na mambo mabali mbali yakiwemo ukosefu wa maghala ya kuhifadhia,ukosefu wa vifungashio,pamoja na baadhi ya vyama ya ushirika kupokea korosho mbichi hivyo kupelekea wanunuzi kugoma kununua na kujikuta wanadaiwa madeni makubwa.

HIVI karibuni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kujionea shughuli mbali mbali za mfumo unaotumika katika uuzaji wa zao la korosho aliweza kubaini kuwepo kwa baadhi ya magunia yaliyokuwa na korosho kuwekewa uchafu wa aina mbali mbali ukiwemo, mawe, mchanga, pamoja na matakataka mbali mbali.

No comments: