Thursday, February 1, 2018

EXIM IMEKABIDHI VITANDA NA MAGODORO 40 KWA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA MBEYA, WODI YA WAZAZI META.

Mkurugenzi Mtendaji was hospital ya rufaa ya Mbeya Dr Godlove Mbwanji akitoa shurkani kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko na mawasiliano wa Benki ya Exim Tanzania, Stanley Kafu (kushoto) baada ya kukabidhiwa msaada wa vitanda na magodoro 40 kutoka benki hiyo jana asubuhi kwa ajili ya wagonjwa katika hospitali hiyo kitengo cha wazazi-Mbeya jijini Mbeya.  Wa pili kulia ni Mkuu wa idara ya wodi ya wazazi-Meta, katika hospitali hiyo Dr John France.

HOSPITALI na kliniki nyingi nchini zina tatizo la ukosefu wa dawa, vifaa na vitanda hasa katika hospitali za rufaa.  Katika kukabiliana na uhaba huu unaosumbua taifa , Exim Bank Tanzania, yenye uwepo wa kimataifa  imeanzisha mradi unaolenga kusaidia upungufu wa vitanda katika hospitali nchini - hivyo benki ya Exim itatoa magodoro and vitanda 500 katika hospitali za serikali katika mikoa 13 nchini kama sehemu ya kampeni yake yenye lengo la kusherehekea miaka 20 ya kutumikia jamii.

Benki ya Exim Tanzania iliadhimisha miaka 20 ya huduma, mwezi wa Agosti mwaka jana, kwa kuzindua mradi wa mwaka mzima unaoitwa “miaka 20 ya kujali jamii” ambao Benki hiyo itawekeza katika sekta ya afya Tanzania. Kama benki ya kiTanzania iliyoanzishwa mwaka wa 1997, Benki ya Exim inafafanua mafanikio kwa jinsi inavyoleta mabadiliko kwa wateja na jamii kwa ujumla.

Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mbeya, ni hospitali ya sita kupokea mchango huu, baada ya Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru, Arusha mwezi uliopita, Hospital ya rufaa Dodoma mwezi Novemba, hospitali ya rufaa Ligula, Mtwara mwezi Oktoba, Hospitali ya Mnazi Mmoja, Unguja, Zanzibar mwezi Septemba na Hospitali ya rufaa Temeke, Dar es Salaam mwezi wa nane mwaka jana. Tukio lilifanyika kwenye hospitali hiyo wodi ya wazazi META na mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa hospitali hiyo Dr. Godlove Mbwanji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa idara ya masoko wa benki ya Exim, Bwana Stanley Kafu alisema, “ Benki ya Exim imekuwa ikisheherekea miaka 20 ya uanzilishi toka Agosti mwaka jana 2017. Kama ishara ya kushukuru  watumishi wake na jamii kwa ujumla, benki imeanzisha mpango wa kutoa vitanda na magodoro kwa hospitali nchini kote kila mwezi. Benki itaendelea mpango huu kwa mwaka mmoja hadi Julai 2018. "

Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali ya rufaa ya Mbeya, Dr Godlove Mbwanji alipongeza Exim Bank Tanzania kwa ahadi yake ya kukabiliana na upungufu wa vitanda kwenye ma hospitali ambao unakabiliwa na taifa na kuleta juhudi zake kwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mbeya. Alisema “Upungufu wa vitanda katika mahospitali ni changamoto kubwa. Msaada huu kutoka benki ya Exim wa hivi vitanda 40 na magodoro utasaidia sana katika kupunguza changamoto hii san a sana kwenye wodi ya wazazi.”

Ikiwa kama sehemu ya mradi wa “miaka 20 ya kujali jamii” benki ya Exim itatoa msaada wa vitanda 500 na magodoro yake kwa hospitali katika mikoa ya Morogoro, Tanga, Dodoma, Kigoma, Kilimanjaro, Mbeya, Arusha, Shinyanga, Mtwara, Pemba na Unguja ambapo mpaka sasa Dar es Salaam, Unguja, Mtwara, Arusha, na Dodoma tayari wameshapokea misaada.

Katika kipindi cha miaka 20 ya kuwepo sokoni benki ya Exim imejenga taasisi imara kijiografia, katika bidhaa za kivumbuzi, mahusiano mazuri na wateja na uwezo wake wa kutoa huduma kwa haraka zaidi.

No comments: