Monday, January 22, 2018

WAJASILIAMALI WATAKIWA KUTUMIA MAFUNZO YA SIDO KIKAMILIFU

Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sporah Lyana akiongea na wajasiliamali mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akifunga mafunzo yaliyokuwa yameandaliwa na SIDO jijini Dar es Salaam yenye lengo la kuwajengea uwezo na kuzipa thamani bidhaa wanazozitengeza. Pembeni yake ni Meneja wa SIDO Dar es Salaam, McDonald Maganga. Picha na Cathbert Kajuna -KAJUNASON/MMG.
Meneja wa SIDO Dar es Salaam, McDonald Maganga akitolea ufafanuzi mafunzo hayo ambayo wamekuwa wakiyatoa kwa wajasiliamali mbali mbali ili kuwajengea uwezo wa kuzipa thamani bidhaa zao wanazozitengeneza. Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sporah Lyana (wa nne kutoka kushoto) na Meneja wa SIDO Dar es Salaam, McDonald Maganga anayemfuatia wakifurahia jambo na wajasiliamali mara baada ya kuhudhuria sherehe ya kufunga kwa mafunzo yao.
Wajasiliamali wakifurahia bidhaa walizozitenegeza wakati wa mafunzo.
Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sporah Lyana akipata maelekezo ya bidhaa walizozitenegeza wakati wa mafunzo. 
Wajasiliamali wakipokea vyeti.

No comments: