Sunday, December 31, 2017

Rais wa Zanzibar Dk. Shein, Ashiriki Katika Zoezi La Usafi Wa Mazingira Katika Nyumba Za Wazee Sebleni Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akishiriki katika zoezi la Usafi wa Mazingira katika eneo la Nyumba za Wazee Sebleni na kujumuika na Wananchi katika zoezi hilo, kulia Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akishiriki katika zoezi la kufanya usafi katika Nyumba za Wazee Sebleni Unguja, kulia Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wazee Vijana Wanawake na Watoto Zanzibar, Mhe. Maudline Cyrus Castico.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Wazee wanaoishi Nyumba za Wazee Sebleni alipofika katika viwanja hivyo kwa ajili ya Uzinduzi wa Usafi wa Mazingira katika eneo hilo
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Vifaa vya Usafi Katibu wa Baraza la Vijana Wilaya ya Magharibi A Unguja Farida Juma, kwa ajili ya zoezi la Usafi katika Wilaya yao, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya Nyumba za Wazee Sebleni wakati wa Uzinduzi wa Zoezi la Usafi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesimama kwa dakika moja kuwakumbuka Wazee waliotangulia mbele ya haki.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Usafi wa Mazingira katika viwanja vya Sebleni Unguja
BAADHI ya Vijana wanaoshiriki katika zoezi la Usafi wa Mazingira katika eneo la Sebleni Nyumba za Wazee wakifanya usafi
WAZEE wa Sebleni wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi wa usafi wa mazingira katika maeneo ya nyumba za wazee sebleni Unguja.
VIJANA wa Mabaraza ya Vijana ya Mkoa wa Mjini Magharibi na Wananchi wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa usafi wa mazingira katika eneo la Nyumba za Wazee Sebleni, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia wakati wa hafla hiyo
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Hamida Mussa Khamis akisoma risala ya Mkoa wakati wa Uzinduzi wa Usafi wa Mazingira katika viwanja vya Nyumba za Wazee Sebleni Unguja.
MKUU wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud, akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kuzungumza na Wananchi walioshiriki kazi ya Usafi wa Mazingira katika viwanja vya Nyumba za Wazee Sebleni.
Picha na Ikulu

No comments: