Tuesday, December 5, 2017

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, JAPHET HASUNGA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KITULO, MAARUFU KAMA BUSTANI YA MUNGU

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kushoto), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakiangalia maua ya asili ambayo ni kivutio kikubwa cha utalii katika hifadhi hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (wa nne kulia), akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy (wa tatu kulia) na baadhi ya viongozi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia), Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa Kitulo, Pius Mzimbe wakiangalia maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Kitulo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akipata maelezo kuhusu maporomoko ya maji ya Mwakipembo ambayo ni kivutio cha utalii ndani ya hifadhi ya Taifa ya Kitulo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Pius Mzimbe wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi hiyo kwenye wilaya ya Makete mkoani Njombe leo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Makete, Veronika Kessy. Pamoja na kivutio hicho hifadhi hiyo ni maarufu duniani kwa kuwa na aina za maua zaidi ya 35 ya asili ambayo hayapatikani kwengineko duniani.
Muonekano mwanana wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. Hifadhi hii ina aina zaidi ya 350 za maua huku aina 35 yakiwa ndwele na hupatikana katika hifadhi hiyo pekee duniani. Vivutio vingine vinavyopatikana katika hifadhi hiyo ni Maporomoko ya maji, ndege aina mbalimbali ambao wengine huama kutoka ulaya wakati wa baridi, wanyamapori aina Swala, Mbega na Nsya. Hata hivyo katika kutimiza mkakati wa Wizara kuboresha vivutio vya utalii, hifadhi hiyo ipo katika maandalizi ya kuanzisha makazi ya Pundamilia na wanyama wengine. Awamu ya kwanza ya kuhamisha pundamiliz 25 kutoka hifadhi ya taifa ya mikumi inatarajiwa kukamilika mwishoni mw mwaka huu. Hifadhi hiyo ni maarufu kwa wenyeji kama 'BUSTANI YA MUNGU'.
Aina mojawapo ya ua ambalo hupatikana katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo, Pius Mzimbe (kushoto) akimuonyesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) sehemu ya eneo lililochaguliwa ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya kuanzisha makazi ya Pundamilia 25 watakaohamishwa kutoka Hifadhi ya Taifa ya Mikumi. Alisema kabla ya mwaka huu kuisha Pundamilia hao watakuwa wameshahamishiwa eneo hilo. Huo ni mkakati wa wizara na Serikali katika kuboresha vivutio vya utalii nchini ili kuongeza idadi ya watalii na mapato.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akisalimiana na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo alipowasili makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe jana.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo makao makuu ya hifadhi hiyo yaliyopo Makete mkoani Njombe. Amewaaka watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na ubunifu, kujiepusha na vitendo vya rusha, kuweka mikakati wa kudhibiti mifugo kuingia hifadhini na sio kusubiri iingie na kuanza kutangaza kuikamata au kuitaifisha, kupunguza malalamiko ya wananchi jirani na hifadhi hiyo, kuongeza idadi ya mapato ya hifadhi na kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga akizungumza na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Kitulo. (Picha na Hamza Temba-Wizara ya Maliasili na Utalii)

No comments: