Sunday, October 29, 2017

TASNIA HALISI WHATSAAP GROUP YAZINDULIWA KWA KISHINDO JIJINI DAR ES SALAAM


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAANDISHI wa habari ambao ni wanachama wa kundi la Whatsapp lijulikanalo kama TASNIA HALISI wamezindua kundi hilo leo Oktoba 28, 2017 kwa sherehe kabambe ya kukata na shoka iliyohanikizwa na nyama choma, vinywaji vya kila aina na muziki.
Mratibu wa shughuli hiyo, Bi. Angela Msangi amesema, kundi hilo ni mukusanyiko wa wanataaluma na wadau wa habari na linalenga kuwaleta pamoja wana tasnia kwa nia ya kubadilishana taarifa na kusaidiana kitaaluma na kijamii.
Katika uzinduzi huo uliosindikizwa na burudani ya muziki umeshuhudia waandishi kutoka sehemu mbalimbali nchini wakishiriki.
Katika sherehe hiyo, shampeni mbili zilifunguliwa ikiwa ni pamoja na kukata keki.























No comments: