Sunday, October 8, 2017

MASAUNI ATEMBELEA MRADI WA UMWAGILIAJI GEREZA LA KILIMO IDETE, ATAKA MKANDARASI ACHUKULIWE HATUA KALI KWA KUUTELEKEZA UJENZI WA MRADI HUO WA MABILIONI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia),


Mkuu wa Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka (kushoto), pamoja na Maafisa wengine wa Jeshi hilo, wakitoka katika Gereza la Kilimo Idete lililopo Ifakara, mara bada ya Naibu Waziri huyo kupokeataarifa ya Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji uliosimama baada ya Mkandarasi kuutelekeza mradi huo wenye thamani ya shilingi Bilioni 2.5. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.


Karani wa Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, Mkaguzi wa Jeshi la Magereza, Juma Mtega, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto),chanzo cha ujenzi wa mradi huo. Masauni alifanya ukaguzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha ambao Mkandarasi aliutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi la Magereza kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.
Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka, akimuonyesha Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), sehemu mbalimbali za Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, wakati Masauni alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi huo wa zaidi ya shilingi Bilioni 2.5 uliosimama baada ya Mkandarasi wa mradi huo, kuutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.


Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akitoa maelekezo kwa viongozi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro ya kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria endapo itathibitika Mkandarasi aliyesimamisha Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, alifanya makosa kwa kusimamisha ujenzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha, tangu mwaka jana 2016. Wapili kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akitoa maelekezo kwa viongozi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro ya kumchunguza na kumchukulia hatua za kisheria endapo itathibitika Mkandarasi aliyesimamisha Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, alifanya makosa kwa kusimamisha ujenzi wa mradi huo wa mabilioni ya fedha, tangu mwaka jana 2016. Kushoto ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Mkoa huo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka.

Mkuu wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Mzee Nyamka, akimfafanuliaNaibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), kuhusu Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji wa Gereza la Kilimo Idete, Ifakara, wakati Masauni alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi huo wa zaidi ya shilingi Bilioni 2.5 uliosimama baada ya Mkandarasi wa mradi huo, kuutelekeza mwaka 2016. Hata hivyo, Masauni alilitaka Jeshi hilo kufanya uchunguzi dhidi ya Mkandarasi huyo na ikithibitika anamakosa akamatwe na achukuliwe hatua za kisheria.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akiwasalimia Maafisa wa Gereza la Kilimo Idete lililopo Ifakara, mkoani Morogoro, wakati kiongozi huyo alipokuwa anawasili katika Gereza hilo kwa ajili ya kuutembelea Ujenzi wa Mradi wa Umwagiliaji uliosimama baada ya Mkandarasi wa Mradi huo kuutelekeza mwaka jana 2016, mradi ambao unathamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 2.5. Gereza hilo linafanya kilimo cha zao la Mpunga na Mahindi.


Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

No comments: