Tuesday, October 24, 2017

KARDINAL PENGO AONGOZA MAASKOFU NA WAOMBOLEZAJI WENGINE KUUAGA MWILI WA ALIYEKUWA ASKOFU WA JIMBO KATOLIKI LA TUNDURU MASASI,ASKOFU CASTORY PAUL MSEMWA

 Askofu Mkuu wa  Jimbo Kuu  Katoliki  la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo akiaga  mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa iliyofanyika katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Katoliki (TEC) Kurasini Jijini Dar es Salaam.
  Askofu Mkuu wa  Jimbo Kuu  Katoliki Tabora, Paul Ruzoka akiaga  mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa iliyofanyika katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
  Katibu wa Rais, Ngusa Samike akiaga mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa iliyofanyika katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya Mapadri nao wakipita mbele kuaga mwili wa Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa mara baada ya Misa katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa likiwa limebebwa na Mapadri wakielekea ndani ya Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 Viongozi mbalimbali, Mapadri, Maaskofu pamoja na waamini wa Kanisa Katoliki wakiwa katika misa ya kumuombea Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa katika Kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Mkuu wa jimbo Kuu la Dodoma Beatus Kinyaiya akizungumza kabla ya kuaga mwili wa marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa katika kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 Askofu Mkuu wa  Jimbo Kuu  Katoliki  Tabora Paul Ruzoka akizungumza katika Misa ya kumuombea Marehemu Askofu Mkuu wa Jimbo la Tunduru na  Masasi Castor Paul Msemwa katika kanisa la Baraza la Maaskofu Kurasini Jijini Dar es Salaam.
 Waumini wa kanisa Katoliki wakiwa katika Ibada ya kumuombea Marehemu katika Kanisa hilo jijini dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Baraza la Maaskofu Tanzania Benard James akizungumza mara baada ya Misa hiyo. Picha na Mpiga Picha wetu.

No comments: