Thursday, September 21, 2017

ZAIDI YA MILIONI 400 KUTUMIKA MRADI MKUBWA WA MAJI KUTOKA ENEO LA PONGWE HADI MUHEZA

Mhandisi wa Mradi wa Maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza kutoka kampuni ya Koberg Construction Co.Limited Mhandisi Stepheni Kingili kushoto akitoa maelekezo kwa Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu namna watakavyoanza kutekeleza mradi huo kuanzia kesho(leo) wakati wa halfa ya makabidhiano ya vifaa vya mradi huo yaliyofanyika ofisi ndogo za mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) eneo la Pongwe
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye ofisi ndogo za mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) kushoto ni Mkurugenzi wa Tanga Uwasa,Mhandisi Joshua Mgeyekwa
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akiingia kwenye halfa hiyo
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa akizungumza katika halfa hiyo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu 
Mbunge wa Jimbo la Muheza(CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza wakati wa halfa hiyo 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza,Luiza Mlelwa akizungumza katika halfa hiyo 
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo akizungumza katika halfa hiyo 
Sehemu ya wagen kutoka maeneo mbalimbali waliojitokeza kushuhudia makabidhiaano haayo 
Sehemu ya wadau waliohudhuria makabidhiano hayo eneo la Pongwe Jijini Tanga
Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajaabu wa pili kutoka kulia akiongozana na baadhi ya viongozi kukagua mabomba yatakayotumikaa kwenye mradi huo kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Luiza Mlelwa na kushoto ni Mhandisi wa Mradi huo ambao utatoa maji Pongwe Jijini Tanga Hadi wilayani Muheza
Moja kati ya vifaa mbalimbali vitakayotumika kwenye mradi huo.
Sehemu ya Mabomba ambayo yatatumika kwenye mradi huo mkubwa utakaogharimu zaidi ya milioni 400 kwa ajili ya kutoa maji eneo la Pongwe Jijini Tanga Hadi wilayani Muheza


WANANCHI wa wilaya ya Muheza mkoani Tanga wataondokana na adha ya huduma ya maji baada ya Serikali kutenga fedha zaidi ya milioni 400 kwa ajili mradi mkubwa wa kutoa maji kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga hadi wilayani Muheza.

Hatua hiyo ina lenga kuondoa changamoto ya uhaba wa maji wilayani Muheza ambayo ilikuwa kikwazo cha maendeleo kwa wananchi kutokana na kutumia muda mwingi kusaka
huduma hiyo badala ya kufanya shughuli za kujiingizia kipato.

Akizungumza jwakati wa kukabidhi mabomba yatakayotumika kwa mkandarasi wa mradi huo katika eneo la Pongwe Jijini Tanga, Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu alisema mradi huo utakuwa ndio mkombozi mkubwa kwa wananchi.

Alisema mradi huo ambao ni mkubwa ni moja kati ya ahadi za Rais John Magufuli alipofanya ziara mkoani Tanga ambapo alihaidi kuhakikisha wakazi wa mji huo wanaondokana na changamoto ya uhaba wa maji.

"Kwanza nimshukuru mh Rais kwa kutekeleza ahadi yake mapema jambo ambalo limetupa faraja kubwa sisi wakazi wa Muheza na vitongoji vyake lakini niwaambie katika mradi huu nitakuwa mkali sana na nitafuatilia kila mwezi kuhakikisha unajengwa kwa viwango kutokana na thamani ya fedha"Alisema.

Aidha alimsisitizia mkandarasi wa ujenzi wa mradi huo kuhakikisha ajira zitakazotolewa ziwalenge vijana waliopo katika maeneo hayo ili kuweza kupunguza ukali na ugumu wa maisha kwao na jamii zinawazunguka.

Awali akizungumza katika makabidhiano hayo,Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Mhandisi Joshua Mgeyekwa alisema mradi huo ni miongoni mwa miradi ya maji inayotarajiwa kutekelezwa wilayani Muheza ili kumaliza tatizo la maji wilayani humo.

Alisema katika mradi huo mamlaka hiyo imetumia zaidi ya milioni 30 katika bajeti zake kufanya tathimini ya mradi huo huku serikali itokea fedha zote ambazo zitatumika katika mradi huo ambao utakwenda sanjari na ujenzi wa tanki la kuhufadhia maji eneo la Kilapura litakalokuwa na ujazo wa lita laki saba.

"Lengo la mamlaka ya maji na serikali ya wilaya ya Muheza pamoja na Mbunge wa Jimbo hilo kuhakikisha wananchi wanaondokana na adha ya huduma ya maji ambayo ndio kilio chao kikubwa kwa wilaya hiyo "Alisema.

Akizungumzia suala la utunzaji wa mradi huo,Mhandisi Mgeyekwa alisema mradi huo ni mali ya wananchi hivyo lazima wahakikishe wanakuwa mabalozi wazuri wa kulinda miundombinu ya maji ili iweze kuwasaidia wao na vizazi vijavyo.

Naye kwa upande wake,Mkandarasi wa Mradi huo kutoka Kampuni ya Koberg Construction Limited,Mhandisi Stephen Kingili alisema mradi huo utatekelezwa kwa wakati ili kuweza kutoa fursa kwa wananchi wa wilaya ya Muheza kuweza kunufuika na huduma hiyo.

Alisema utekelezaji wa mradi huo utaanza kutekelezwa kesho (Septemba 21) ambao utakamilika Mei 19 mwakani ukichukua miezi 8 ili kuweza kukamilika na hivyo wananchi kuweza kuutumia.

Aidha alisema mradi huo utakuwa na urefu wa km 16.9 kutoka eneo la Pongwe Jijini Tanga mpaka Muheza mjini ambao utakwenda sambamba na maungio ya kuchepusha maji katika vijiji vyote utakaopita ili kuwarahisishia wananchi kuweza kujiunganishia huduma hiyo pindi wanapokuwa wakihitaji.

Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: