Sunday, August 20, 2017

MTANDAO WA ELIMU TANZANIA WAHITIMISHA KUTOA MAFUNZO KWA WADAU WA ASASI ZA ELIMU KWA MIKOA SITA MORO



Afisa miradi ya elimu kwa masharika yasiyo ya kiserikali ubalozi wa Sweden nchini, Stephen Chimalo akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya ufuatiliaji hatua ya chini ya uandaaji wa bajeti na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika sekta ya elimu kwa kutumia mfumo wa PETS kwa wadau kutoka asasi za elimu kwa mikoa ya Tanga, Tabora, Dodoma, Singida, Dar es Salaam na wenyeji Morogoro iliyoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met).
Afisa miradi wa Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met), Alistidia Kamugisha akizungumza jambo katika mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku tatu hoteli ya Flomi mkoani Morogoro.
Mtaalamu wa masuala ya IT Mtandao wa elimu Tanzania, Dominic Dogani akifafanua jambo kwa wadau wa mafunzo hayo wakati wa kujadili mada kupitia vikundi.
Mwanaidi Juma (Katikati) kutoka shirika la Morogoro Saving The Poor Organization (Mosaporg) akiwa na wadau wenzake wa elimu wakati wakiwajibika katika majukumu ya kujifunza mafunzo hayo.

Mratibu wa shirika la Youth Movement For Change (YMC) la mkoani Singida, Fidelis Yonde kushoto akijadiliana jambo na washiriki wa mafunzo hayo.
Mkufunzi wa masuala ya elimu, Zelote Loilang'akaki akitoa mafunzo kwa wadau wa asasi za elimu yaliyoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met) ya namna ya kufuatilia hatua ya chini ya uandaaji wa bajeti na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika sekta ya elimu kwa kutumia mfumo wa PETS kwa mikoa ya Tanga, Tabora, Dodoma, Singida, Dar es Salaam na wenyeji Morogoro iliyoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met).

Mratibu wa shirika la Youth Movement For Change (YMC) la mkoani Singida, Fidelis Yonde akielezea jambo kuhusu masuala ya changamoto cha elimu ya Tanzania.
Mkurugenzi Mtendaji Fair Education & Information Centre (Fadice) kutoka mkoa wa Tabora Tabora, Philimon Boyo akifafanua jambo.

Baadhi ya wadau kutoka asasi za elimu kwa mikoa ya Tanga, Tabora, Dodoma, Singida, Dar es Salaam na wenyeji Morogoro wakifutilia mafunzo ya ufuatiliaji hatua ya chini ya uandaaji wa bajeti na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika sekta ya elimu kwa kutumia mfumo wa PETS yaliyoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met).
Kiongozi wa shirika la Tabora Advocacy Centre For Development (Tacede), Pai Nyanzandoba akiwalisha mada baada ya washiriki wa mafunzo hayo kujadiliana kwenye vikundi katika siku yao ya tatu ya mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Morogoro.
Godbless Nkungu kutoka shirika la Youth Life Relief Foundation (YLRF) Tabora naye akiwalisha mada mara baada ya washiriki wa mafunzo hayo kujadiliana kupitia vikundi.
Naye Mkurugenzi Mtendaji Fair Education & Information Centre (Fadice) akiwasilisha mada kupitia kundi lake wakati wa mafunzo hayo.Afisa miradi ya elimu kwa masharika yasiyo ya kiserikali ubalozi wa Sweden nchini, Stephen Chimalo wa pili kutoka (kulia mstari wa mbele waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wadau kutoka asasi za elimu kwa mikoa ya Tanga, Tabora, Dodoma, Singida, Dar es Salaam na wenyeji Morogoro mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo ya ufuatiliaji hatua ya chini ya uandaaji wa bajeti na ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika sekta ya elimu kwa kutumia mfumo wa PETS kwa iliyoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Ten/Met).

No comments: