Tuesday, August 8, 2017

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN ATEMBELEA BANDA LA NIDA; AFURAHISHWA NA HATUA ZA USAJILI

Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye Banda la maonyesho la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA). Makamu wa Rais alipokelewa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi. Rose Mdami


Makamu wa Rais anapokea taarifa ya shughuli za Usajili ambazo zimekuwa zikifanyika katika Banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wakati wa Maonyesho ya Nanenane kwenye Viwanja vya Ngongo – Lindi.
Makamu wa Rais akikagua Vitambulisho vinavyogawanywa kwa wananchi Wananchi wakati wa maonyesho ya Nanenane mkoani Lindi.

Mhe. Makamu wa Rais akikagua fomu za Usajili zinavyohakikiwa kabla ya mwananchi kuchukuliwa alama za Vidole, Picha na Saini ya Kielektroniki.
Makamu wa Rais akikagua mashine za Usajili zinazotumika kuwasajili wananchi; ikiwemo uchukuaji wa alama za kibaiolojia, Picha na Saini ya Kielektroniki
Watumishi wa NIDA wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kupata ushindi kwenye maonyesho ya Nanenane kwa mwaka 2017.

No comments: