Thursday, July 20, 2017

RC SHINYANGA AKUTANA NA WAWEKEZAJI NA WAFANYABIASHARA WA MKOA WA SHINYANGA


Alhamis Julai 20,2017 Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack amekutana na wawekezaji na wafanyabiashara wa mkoa wa Shinyanga kwa lengo la kufahamiana na kujadili mambo kadha wa kadha ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika mkoa wa Shinyanga.



Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga na kukutanisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka wilaya zote za mkoa wa Shinyanga.



Akizungumza katika kikao hicho,Telack alisema huu ni mwaka wa pili wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa miaka mitano 2016/2017 – 2020/2021 wenye dhima ya kujenga uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya maendeleo ya watu.



“Ili kutimiza malengo ya mpango huu lazima serikali ifanye kazi kwa ushirikiano wa karibu na sekta binafsi na nyinyi ni sehemu ya sekta binafsi na ili kudumisha ushirikiano huo serikali imeanzisha mabaraza ya biashara katika ngazi ya taifa,mikoa na wilaya”,alieleza Telack.



Aidha alisema uwekezaji ni moja ya shughuli zinazochochea kasi ya ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla ambapo hadi sasa mkoa huo una jumla ya viwanda 81,ambapo viwanda vikubwa ni 18,viwanda vya kati 9 na vidogo 54.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akitoa hotuba yake wakati wa kikao chake pamoja na wawekezaji na wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga leo Alhamis Julai 20,2017.
Wafanyabiashara,wawekezaji na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwa ukumbini  Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza katika kikao hicho ambapo aliwahamasisha wafanyabiashara kushirikiana na kupeana fursa mbalimbali
Kaimu Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Jackton Koy akizungumza katika kikao hicho.  Kushoto ni Kaimu Mwenyekiti wa wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Jackton Koy,katikati ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack akifuatiwa na katibu tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela.
Kikao kinaendelea
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akichangia hoja katika kikao hicho  Wawekezaji na wafanyabiashara wakiwa katika kikao.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba akichangia hoja ukumbini
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga,Said Pamui akizungumza katika kikao hicho  Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Muliro Jumanne Muliro aliyehamishiwa mkoa wa Kinondoni akizungumza ukumbini.
Kikao kinaendelea
a
Mkurugenzi wa SHUWASA Injinia Sylivester Mahole akichangia hoja ukumbini.
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akizungumza katika kikao hicho.
 Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila akichangia hoja ukumbini.
Wafanyabiashara na wawekezaji wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Kikao kinaendelea  Mkurugenzi wa Hasmukh Group, Kishan Hasmukh akichangia hoja wakati wa kikao hicho.
Meneja wa Ustawi wa Jamii na Kampuni ya Acacia Bulyanhulu,Elias Kasitila (kushoto) na Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mkanza wakiwa katika kikao hicho
Wawekezaji wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini.
Kikao kinaendelea
Kikao kinaendelea.
Wadau wakiwa ukumbini
Mwekezaji Gilitu Nila Makula akizungumza ukumbini.
Mkurugenzi wa Soud Group,Hilal Soud akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Katibu wa Wafanyabiashara mkoa wa Shinyanga Macelina Lauo akizungumza wakati wa kikao hicho.  Meneja Uendelevu mgodi wa Buzwagi George Mkanza  akifuatilia kwa umakini kilichokuwa kinaendelea ukumbini.

Tunafuatilia kinachoendelea....
Mwenyekiti wa waendesha bodaboda manispaa ya Shinyanga Wenceslaus Modest akichangia hoja
Kikao kinaendelea
Picha zote Kadama Malunde - Malunde1 blog

No comments: