Sunday, June 11, 2017

WATANZANIA WATAKIWA KUBADILI FIKRA KUFIKIA UCHUMI WA VIWANDA

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama kushoto  akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Dk. John Jingu (katikati) na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,  Bi. Beng Issa kulia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la  Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama kushoto  akikata utepe(ribbon) kuashiria kuzindua wa taarifa ya utekelezaji wa sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ya Julai 2015 mpaka April 2017 wakati wa Kongamano la Pili la  Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi,(katikati) Mwenyekiti wa Bodi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Dk. John Jingu na kulia ni  Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi. Beng’i Issa.  
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama kushoto  akionyesha kitabu cha taarifa ya utekelezaji wa sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ya Julai 2015 mpaka April 2017 mara baada ya kuzindua taarifa hiyo wakati wa Kongamano la Pili la  Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi,(katikati) Mwenyekiti wa Bodi wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Dk. John Jingu na kulia ni  Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Bi. Beng’i Issa.  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama kushoto  akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Joel Bendera  taarifa ya utekelezaji wa sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ya Julai 2015 mpaka April 2017 mara baada ya kuzindua taarifa hiyo wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Pili la  Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC),Bi. Beng Issa.

Watanzania wametakiwa kubadili fikra za kimtanzamo na kila mtu kutimiza wajibu wake kwa lengo la kuunga mkono dhamira ya serikali ya  awamu ya tano ili kujenga uchumi wa viwanda na kuboresha ustawi wa jamii.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira na Walemavu Jenista Mhagama alisema hayo wakati alipokuwa akifungua Kongamano la Pili la  Uwezeshaji Watanzania Kiuchumi, kuwa watanzania wanatakiwa kubadili fikra za kimtanzamo ili kuweza kufikia uchumi wa viwanda, na kuboresha ustawi wa jamii.

“ Nchi yetu imeamua kubadilisha mwelekeo wa uchumi wa nchi yetu na sisi tunawajibu wa kubadili fikra za kimtanzano ili kufikia uchumi wa viwanda,” aliongeza kusema Bi. Mhagama, ambaye alifungua kongamano hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Pia aliwataka washiriki wa kongamano kwenda kushirikiana na wananchi katika kuhakikisha suala la uchumi wa wananchi unakuzwa. Na aliwasisitiza watumishi wa umma kuwa mfano katika kuchochea dhamira hiyo kwa kufanya kazi kwa vitendo.

Alisema serikali imeweka mikakati kabambe ya kuandaa nguvu kazi yenye ujuzi  inayoendana na soko la ajira kupitia program mbalimbali ikiwemo ya kuwafundisha vijana ujuzi waweze kutumika katika nguvu kazi. Na aliwataka wakuu wa mikoa yote kuainisha fursa za kiuchumi na kumpatia waziri mkuu ili zifanyiwe kazi.

Halikadhalika aliitaka mifuko yote ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kuhakikisha fedha zilizopo katika mifuko yao inawafikia watanzania waweze kukopa na kuwekeza katika shughuli za uzalishaji na biashara. Kauli Mbiu ya Kongamano hilo ni Wezesha Watanzania Kushiriki Uchumi wa viwanda.

Waziri huyo pia alizidua taarifa ya utekelezaji wa sera ya taifa ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ya julai  2015 mpaka April 2017. Pia alitoa vyeti na vikombe kwa sekta umma na binafsi waliofanya vizuri katika kutekeleza uwezeshaji wananchi kiuchumi. 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la  Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi  (NEEC),Bi. Beng’I Issa alisema kongamano hilo lilikuwa la mafanikio kwa kuwa lilishirkisha wadau wote na kwa sasa wanalenga kwenda kutekeleza kwa vitendo majukumu yao. 

“Kongamano hili tumepatiwa agizo la kila Wilaya kuwa na kiwanda kimoja na sisi tumejipanga kusimamia kwa vitendo,” na kuongea  kusema viwanda huwezesha mali ghafi kuongezwa thamani na kutoa ajira.

Sambamba na hilo huongeza uzalishaji katika sekta ya kilimo na kuwa chachu ya uchumi wa nchi kwa kuwa kilimo kina nafasi ya kuajiri watu wengi zaidi na kuongeza vipato vya wananchi.

Pia kila halmashauri imepwa jukumu la kuainisha maeneo ya kufanyia biashara zikiwa na miundombinu yote na kumpatia waziri mkuu hadi ifikapo Agosti 2017 ili yaweze kufanyiwa kazi.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius K. Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJKNUAT), Profesa Dominic Kambarage alisema baraza linafanya kazi kubwa na nzuri na inatekeleza sera ya uwezeshaji wananchi kiuchumi.

”Kutokana na kazi hii nzuri tuongeze nguvu ngazi ya mikoa na wilaya za kufanya kazi kwa vitendo na maeneo ya biashara yatengwe wananchi wawe na fursa za maeneo ya kufanyia biashara,”. Na taasisi za elimu ya juu na kati ziboreshe mitaala yao kwa ajili ya vijana kuondoa tatizo la ajira.

No comments: