Monday, June 19, 2017

SPIKA NDUGAI AONGOZA WABUNGE KATIKA HARAMBEE YA UJENZI WA JENGO LA JUMUIYA YA KIKRISTO TANZANIA TUKIO LILILOFANYIKA LEO MJINI DODOMA.



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, katika tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma, Spika Ndugai pia ni Mgeni rasmi na aliongoza Wabunge katika harambee hiyo. 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (kushoto) kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, katika tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma. katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)akiongoza Wabunge Mbali mbali kucheza nyimbo ya injili kama njia moja wapo ya kuhamasisha uchangiaji kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza jambo kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma. kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda na katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa 
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akiteta jambo na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma, Pia Spika Ndugai aliongoza Wabunge katika harambee hiyo. 
Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (kushoto) akisalimiana na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, katikati ni Ndg. Elton Mapesa Mwakilishi wa Harambee kutoka External, Ubungo Jijini Dar es Salaam. Katika harambee hiyo, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai aliwaongoza wa Bunge katika uchangiaji wa ujenzi wa jengo hilo. 
Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (wa pili kushoto) akizungumza jambo baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, kulia ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah, kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa na wa pili kulia ni Ndg. Elton Mapesa Mwakilishi wa Harambee kutoka External Ubungo Jijini Dar es Salaam.

No comments: