Friday, June 9, 2017

RC ANNA MNGWIRA ATEMBELEA FAMILIA YA DKT NDESAMBURO,AZUNGUMZA NA WANACCM KILIMANJARO.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akizungumza na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi alipotembelea ofisi za chama hicho kujitamburisha .kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma ,na anayefuatia ni Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi,Aisha Amour.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Manispaa ya Moshi,Elizabeth Minde (katikati) akifurahia jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira (hayupo pichani) alipokutana na uongozi wa chama hicho katika ofisi za CCM-Mkoa wa Kilimanjaro.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro ,Idd Juma akitoa neon la shukrani mara baada ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mngwira kutembelea ofisi za chama hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira akitoka ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro mara baada ya kuonana na viongozi wa chama hicho.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna mngwira akisalimaiana na Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Kilimanjaro alipofika nyumbani kwa Marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo kutoa pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mngwira akisalimiana na mtoto wa Marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo ,Sindato Ndesamburo alipotembelea nyumbani kwa marehemu kutoa pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akitia saini katika kitabu cha waombolezaji mara baada ya kufika nyumbani kwa Marehemu Dkt Ndesamburo kutoa salamu za pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna mngwira akizungumza jambo na mjane wa Marehemu Dkt Ndesamburo ,Ndehorio Ndesamburo alipofika nyumbani kutoa salamu za pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,akitembelea kaburi ulipolazwa mwili wa marehemu Dkt Philemoni Ndesamburo alipofika nyumbani kutoa salamu za pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akiongoza sala katika kaburi la marehemu Dkt Philemon Ndesamburo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira akimpa mkono wa pole Mbunge wa viti maalumu na mtoto wa marehemu Dkt Ndesamburo ,Lucy Owenya alipofika kutoa salamu za pole kwa familia y marehemu.
Mbunge wa Viti Maalum Chadema mkoa wa Kilimanjaro,Lucy Owenya akizungumza jambo na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira alipofika kutoa salamu za pole kwa familia.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akisalimiana na wananchi katika neo la Kwa Alphonce wakati akiwa njiani akitoka kutoa salamu za pole kwa familia ya Dkt Ndesamburo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akiwa katika picha ya pamoja na wananchi alipowasalimia katika eneo la Kwa Alphonce mjini Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro akizungumza na mmoja wa wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro aliposhuka kwenye gari kuwasalimia.
Na Dixon Busagaga wa Busagaga's Orijino Blog.

No comments: