Tuesday, May 30, 2017

WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO YAWASILISHA BAJETI YAKE BUNGENI MJINI DODOMA



Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi (Bajeti) ya Wizara yake ya zaidi ya shilingi trilioni 11.757, Bungeni Mjini Dodoma ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote 9 yaliyo chini ya Wizara hiyo.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi (Bajeti) ya Wizara yake ya zaidi ya shilingi trilioni 11.757, Bungeni Mjini Dodoma ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote 9 yaliyo chini ya Wizara hiyo.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi (Bajeti) ya Wizara yake ya zaidi ya shilingi trilioni 11.757, Bungeni Mjini Dodoma ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote 9 yaliyo chini ya Wizara hiyo.
Viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake, wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo, Bungeni Mjini Dodoma, ambapo kiasi cha shilingi trilioni 11.757 kimeombwa ili Wizara hiyo iweze kutekeleza majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo kwa mwaka wa Fedha 2017/2018.
Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa akimpongeza Mhe. Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kwa uwasilishaji makini wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban, akimpongeza Mhe. Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), kwa uwasilishaji makini wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango, akisalimiana na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Mhe. Peter Serukamba, mara baada ya Waziri Mpango kuwasilisha Bajeti ya Wizara hiyo Bungeni Mjini Dodoma ambapo ameliomba Bunge liidhinishe makadirio ya Mapato na Matumizi ya shilingi trilioni 11.757 ya Wizara hiyo.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akisalimiana na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Juma Assad, kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Manaibu Katibu wakuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Amina Khamis Shaaban, na Bi. Dorothy Mwanyika, wakibadilishana mawazo nje ya Ukumbi wa Bunge Mjini Dododma mara baada ya kuwasilishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo ambapo kiasi cha shilingi trilioni 11.757 zinatarajiwa kukusanywa na kutumiwa na Wizara ya Fedha na Mipango.
Viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Taasisi zake, wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (wa tano kushoto), nje ya ukumbi wa Bunge mara baada ya kuwasilishwa kwa Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo. (Picha zote na
…………………………..

Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma

Wizara ya Fedha na Mipango imeliomba Bunge iidhinishie makadirio ya mapato na matumizi (Bajeti) ya zaidi ya shilingi trilioni 11.757 ili iweze kutekeleza majukumu yake kwa mwaka wa fedha 2017/2018, kwa mafungu yote 9 yaliyochini ya Wizara hiyo.

Maombi hayo yametolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango, wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizaya hiyo, Bungeni Mjini Dodoma, leo.

Dkt. Mpango amesema kuwa kati ya fedha hizo, shilingi trilioni 10.328 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na shilingi trilioni 1.429 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

Amefafanua kuwa Matumizi ya Kawaida yanajumuisha shilingi bilioni 87.996 kwa ajili ya mishahara, shilingi bilioni 778.612 kwa ajili ya matumizi Mengineyo (OC) na shilingi trilioni 9.461 ni kwa ajili ya kulipa Deni la Taifa na Huduma nyingine.

Aidha, katika fedha za matumizi ya maendeleo, shilingi trilioni 1.382 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 46.108 ni fedha za nje.

No comments: