Wednesday, May 24, 2017

WASICHANA 8000 KUNUFAIKA NA MRADI WA UNESCO WA ELIMU

Wasichana 8,000 waliopo shuleni na 600 ambao hawako shuleni watanufaika na mradi mkubwa wa kuwawezesha wasichana na wanawake vijana kupata elimu. Mradi huo wa miaka minne wenye gharama ya dola za Marekani milioni 5 utafanyika katika wilaya tano nchini. Wilaya hizo ni Ngorongoro, Kasulu, Sengerema, Micheweni na Mkoani. Mradi huo ambao upo hatua ya pili umeanza kwa kongamano lililofunguliwa jana na Katibu Mkuu wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Dk Leonard Akwilapo.  Mgeni rasmi kwenye kongamano hilo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt Leonard Akwilapo akifungua rasmi kongamano la viongozi mbalimbali wa wizara na wilaya tano nchini kujadili na kupanga mikakati ya namna bora ya kuwawezesha wasichana na wanawake vijana katika wilaya husika kupata elimu katika kipindi cha miaka minne ijayo.

Mradi huo mkubwa kwa mujibu wa Katibu mkuu huyo umelenga kuwaokoa wanafunzi kabla hawajakumbwa na matatizo yanayokatisha masomo yao. Aidha utawapa fursa za kuboresha zaidi mafunzo mbalimbali waliyonayo ambao utawafanya kuwa watu wazuri zaidi katika jamii na hivyo kuchangia maendeleo ya taifa na jamii walizopo. 

 Katibu mkuu huyo ambaye alifungua kongamano na kuzindua mradi huoi awamu ya pili alisema kwamba ni matumaini yake kwamba jamii itaukumbatia mradi huo ili kuwa na taifa lenye mafanikio makubwa katika malengo ya maendeleo endelevu ya dunia kwa kuzingatia lengo namba tano.  Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akitoa neno la ufunguzi katika kongamano la viongozi mbalimbali wa wizara na wilaya tano nchini kujadili na kupanga mikakati ya namna bora ya kuwawezesha wasichana na wanawake vijana katika wilaya husika kupata elimu katika kipindi cha miaka minne ijayo.

 Amewataka wazazi na vijana kutimiza wajibu wao kwa kubadilika kitabia na kutambua umuhimu wa elimu katika kufanikisha wanachotaka ambacho ni maendeleo binafsi , familia na taifa kwa ujumla. Katika hotuba yake alisema ni matumaini kwamba wadau katika mradi huo watafaikisha katika kipindi cha miaka minne mipango yote iliyolenga kuboresha huduma kwa wasichana na wanawake vijana, kushawishi jamii kubadilika na kuachana na tamaduni mbaya kama ndoa za utotoni na ukeketaji. 

 Naye Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na utamaduni UNESCO, Zulmira Rodrigues alisema mradi huo ulioanza mwaka jana na kufanyiwa tathmini umeonesha changamoto kubwa ya watoto wa kike ikiwamo mimba za utotoni,ukeketaji na kushindwa masomo.  Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la misaada Korea International Cooperation Agency (KOICA) nchini, Joonsung Park akitoa neon kuhusu ufadhili wa KOICA ambao imeutoa katika mradi huo na mipango yao ya kusaidia Tanzania.

 Alisema lengo la mradi ni kuhakikisha kwamba mwanamke anapata fursa za kupambana katika mazingira yake kama anavyofanya mwanaume kwa kuwezeshwa na kuzuia mila, tabia na tamaduniu mbaya ambazo zinakwamisha uwezo wake wa kuhudhuria masomo.

 Aidha alisema mradi huo utatoa nafasi kwa wanawake vijana ambao wamekosa masomo au wameacha masomo au hawakwenda shule kabisa kupata nafasi ya kusoma. Mradi huo unaofadhiliwa na Shirika la kimataifa la misaada la Korea (KOICA) kupitia UNESCO na kufanyiwa kazi pia na mashirika ya UN Women na UNFPA unaangalia namna bora ya kukabiliana na changamoto za mabinti wanaokwenda shule katika wilaya hizo ili kuwawezesha kuwa watu bora katika jamii siku za usoni.  Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu (UNFPA) nchini, Dk. Hashina Begum akitoa neno kwa niaba ya UNFPA.

 Mradi huo ni sehemu ya mradi wa Global Initiative unaoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, sayansi na Utamaduni (UNESCO), Shirika la Mpango wa watu (UNFPA) na Shirika la Umoja wa mataifa la wanawake(UN Women) wa kuwawezesha wanawake kupitia elimu uliozinduliwa katika nchi sita duniani. Awamu ya kwanza ya mradi huo umelenga kufanywa katika nchi tatu za Mali, Nepal na Tanzania na ulitiwa saini mwaka jana, 2016. Katika mradi huo serikali ya Tanzania inawakilishwa na Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto; na Wizara ya Katiba na Sheria ambayo ikiratibu mradi kwa niaba ya serikali ya Tanzania. Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN Women) Tanzania, Bi. Hodan Addou akitoa neno kwa niaba ya UN Women.

 Aidha UNESCO inatekeleza mradi huo kwa kushirikiana na UNFPA na UN Women. Katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa KOICA Tanzania, Joosung Park pia alizungumza umuhimu wa kufundisha watoto wa kike na kuwapa fursa na kusema kwamba unapofunza wanawake unafunza taifa huku akisema kwamba wazazi wanahusika sana katika hilo akitolea mfano waziri wa mambo ya nje wa Korea wa sasa ambaye ni mwanamke kwa mara ya kwanza katika miaka mingi ya historia ya nchi hiyo. 

 Mzungumzaji mwingine ni ambaye alikuwa Mwakilishi wa UNFPA Tanzania, Dk Hashina Begum alitaka jamii kuhakikisha kwamba inatoa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana ili kuzuia uzazi usiokuwa na mpango ambao unakwamisha maendeleo. Anna Holmström kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) akitoa maelezo kuhusu mradi huo kwa washiriki waliohudhuria kongamano hilo.[/caption] [caption id="attachment_2196" align="aligncenter" width="1299"]Picha juu na chini ni Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo. [Washiriki wa kongamano la viongozi mbalimbali wa wizara na wilaya tano nchini kujadili na kupanga mikakati ya namna bora ya kuwawezesha wasichana na wanawake vijana katika wilaya husika kupata elimu katika kipindi cha miaka minne ijayo wakiwa kwenye picha ya pamoja.

No comments: