Sunday, May 14, 2017

ULEGA AWATEMBELEA WANANCHI WA TAMBANI WALIOKOSA MAWASILIANO BAINA YA KIJIJI NA KIJIJI

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega amewatembelea wananchi wa Kijiji Tambani ambao hawana mawasiliano ya kuvuka kwenda kutokana na daraja kuchukuliwa na maji.

Akizungumza na wananchi cha Tambani, Ulega amesema kuwa mvua hizo zimeleta athari hivyo unahitajika ufumbuzi wa haraka.

Amesema usafiri wa mitumbwi si salama katika kutoa huduma ya usafiri kwa wananchi wa kijiji cha tambani na maeneo mengine. Kutokana na wananchi hao kukosa mawasiliano Mbunge huyo ametoa sh.milioni moja pamoja na mifuko ya saruji 100 ili kuweza kutengeneza daraja hilo.

Wananchi wa kijiji hicho kwa kila kaya wamekubalina kutoa sh.10,000 ambazo zitafanya kazi katika ujenzi wa daraja hilo pamoja na nguvu zao zitatumika. Diwani wa Tambani, Ally Mtamilwa amsema kuwa ujio wa Mbunge wa jimbo la Mkuranga ameeta matumaini kwa wananchi na kuahidi nae kutoa mifuko 20 ya saruji.
Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika kivuko ambacho si salama kuelekea upande wa pili alipotembelea kijiji cha tambani ambao wamekosa mawasiliano leo.

Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akiwa katika kivuko ambacho si salama kuelekea upande wa pili alipotembelea kijiji cha tambani ambao wamekosa mawasiliano leo.
Wananchi wakiwa katika kivuko ambacho si salama kwa safari baada daraja la kijiji hicho kusombwa na maji leo kufuatia mvua iliokuwa ikinyesha maeneo mbalimbali nchini.
Wananchi wakisubiri kivuko ambacho si salama na kuwagharimu kulipa sh.500 kwa kila safari wanayoifanya kwenda katika vijiji vingine kupata mahitaji .(picha na Emmanuel Massaka Globu ya Jamii )

Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akizungumza na wananchiwa wa kijiji cha Tambani ambao wamekosa mawasiliano kutokana na daraja kuchukuliwa na maji leo.
Diwani wa Tambani , Ally Mtamilwa akizungumza na wananchi wake wakati wa ziara ya mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega.
Mbunge wa Mkuranga , Abdallah Ulega akikabidhi msaada wa sh.milioni moja kwa ajili ya ujenzi wa daraja lilichukuwa na maji katika kijiji cha Tambani.

No comments: