Tuesday, May 9, 2017

SERIKALI KUBORESHA KIWANGO CHA VYOO BORA KUFIKIA 2025


Na Ally Daud-WAMJW DODOMA
SERIKALIi imedhamiria kuboresha kiwango bora  vyoo mjini na vijijini  kutoka asilimia 35 hadi asilimia 55 kufikia mwaka 2025 ili kujenga taifa lenye afya bora na lisilo na maambukizi ya magonjwa yatokanayo na uchafu wa vyoo.
Akizungumza hayo kwenye uzinduzi wa  kampeni ya utunzaji wa mazingira ijulikanayo kama “NIPO TAYARI” Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali imepania kufikisha asilimia ya ubora wa vyoo mpaka kufikia 2030.
“Hatua hii itafikiwa endapo kwa pamoja tutasukuma mbele ajenda ya usafi wa mazingira kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hasa katika ujenzi wa vyoo bora,utupaji salama wa taka ngumu,upatikanaji wa maji salama kwa mikono miwili” alisema Waziri Ummy.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa yapo mafanikio yaliyofikiwa katika kupunguza kasi ya watu kujisaidia ovyo tabia ambayo ni kisababishi cha maambukizi ya magonjwa mengi katika jamii.
Mbali na hayo Waziri Ummy alitoa rai kwa wanasiasa wenginekushirikiana na wananchi katika majimbo yao ilikusukuma kwa vitendo ajenda ya Usafi wa Mazingira  nchini .
Kwa upande wake Naibu waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Bw. Suleiman Jaffo amesema kuwa  watanzania wa wa mijini na vijijini wawe mstari wa mbele katika kuhakikisha wanatumia vyoo bora kila kaya ili kuepuka magonjwa ya kuambukiza.

Naye Naibu Waziri wa maji na umwagiliaji Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuwa ili kuendana na kasi hiyo wamejipanga kuhakikisha shule zote za msingi na sekondari nchini zinapata maji safi na salama kwa wakati sahihi.

No comments: