Wednesday, May 24, 2017

MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI WATOA ELIMU KATIKA MIKOA YA DODOMA, MOROGORO, KILIMANJARO NA ARUSHA

 Mjumbe wa Bodi wa  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Francis Michael akifungua Semina ya uelimishaji kwa Waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo (jana), kulia ni Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu.
 Mwanasheria Mwandamizi Bi. Irine Mungu kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi jijini Morogoro leo.
 Afisa Uhusuano Mwandamizi kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) akitoa mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi mkoani morogoro leo.
 Bw. Fabian Felician akichangia mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi iliofanika mkoani Morogoro leo.
 Afisa Kazi Mfawidhi mkoa wa Morogoro Bw. Simbo Swai akichangia mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi iliyofanyika mkoani Morogoro leo.
 Bi. Hilda Msemo kutoka Mzinga Corporation akichangia mada katika semina ya uelimishaji kwa waajiri kuhusu haki na wajibu wa mwajiri na mfanyakazi iliyofanika mkoani Morogoro leo.
Baadhi ya washiriki wa semina ya uelimishaji kwa waajiri wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa semina hiyo ambaye ni Mjumbe wa Bodi wa  Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Dkt. Francis Michael mkoani Morogoro leo.

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), umeendesha semina ya siku moja kwa waajiri nchini katika mikoa minne, ili kutoa elimu juu ya shughuli za Mfuko na wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi wao katika kujisajili na kuwalipa michango kwa niaba ya waajiriwa wao.

Akizungumza katika semina hiyo mjumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko Dkt. Francis Michael .
Amesema kuanzishwa kwa mfuko huo kumekuja wakati muafaka ambapo Tanzania inaelekea katika uchumi wa viwanda hivyo kupelekea ongezeko la wafanyakazi ambapo chombo hicho ndio mkombozi wa majanga yatokanayo na kazi.                

“Ni muda muafaka kwa waajiri kutambua wajibu wenu katika Mfuko huu na pia kutambua madhara ya kutotekeleza wajibu wenu” Alisema Dkt. Michael.

Katika hotuba yake, Dkt. Michael alieleza umuhimu wa waajiri kuwalipia michango wafanyakazi wake kama sheria inavyotaka, ili kuwawekea akiba pindi wapatapo na majanga wakiwa kazini.

Mfuko wa Fidia kwa wafanyakazi ni Taasisi ya Serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na umeundwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi Sura ya 263 iliyorejewa Desemba, Mwaka 2015.

Dkt. Michael amesema, Mfuko umeamua kuandaa semina hiyo ili kutoa elimu zaidi kwa waajiri  kwa kutambua kuwa waajiri ndio wadau wakuu wa Mfuko huo na semina hiyo itawasaidia kujua kazi za Mfuko lakini pia wajibu wa waajiri kwa wafanyakazi katika kutoa michango ya kila mwezi.

Akitoa mada juu ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Sebera Fulgence, alisema, Mfuko huo upo kisheria ili kutoa fidia kwa wafanyakazi watakaoumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi.

Naye Mwanasheria Mwandamizi wa Mfuko huo Bi.Irene Mungure amesema, ni muda mwafaka kwa waajiri kutambua wajibu wao katika mfuko ikiwa ni pamoja na kutambua madhara ya kutokutekeleza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria.

 Katika uzinduzi wa semina hizo jana Makao Makuu ya Nchi Dodoma, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Emmanuel Humba, alifafanua zaidi juu ya haja ya waajiri kuufahamu vizuri Mfuko namna unavyoendeshwa ikiwa ni pamoja na kulipa fidia kwa wafanyakazi watakaoumia, kuugua ama kufariki. Aidha, alisema kuwa waajiri ni wadau wakuu wa uendelezaji Mfuko.

Bw. Humba aliwaasa waajiri kutokufanya udanganyifu  na ubadhilifu hasa katika uwasilishwaji wa michango kwani itakuwa ni kuudidimiza Mfuko na ni kosa kisheria na waajiri watakaojihusisha watachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi Sura ya 263 iliyorejewa Desemba, Mwaka 2015.

Semina hiyo imefanyika katika mikoa ya Dodoma,Kilimanjaro, Morogoro na Arusha.

No comments: