Tuesday, March 21, 2017

WANANDOA KUACHANA KWA MKATABA MAALUM BILA KWENDA MAHAKAMANI


Na  Bashir  Yakub
Zipo  namna  nyingi  za  kuachana  kisheria  kwa  wanandoa  ambao  wanadhani  sasa hawawezi  kuendelea. Wengi  wetu  tunajua  zile  za  kupitia mahakamani.  Zile  ni  sahihi  lakini  upo  uwezekano  pia wa  kuachana  kwa  mkataba  maalum  bila  kuhitaji  kwenda  mahakamani.
Aidha  yafaa  ifahamike  kuwa  Kuachana  katika  ndoa  na  kuamua  kuishi   nje  ya  ndoa  ni  jambo  la  kawaida.  Kisheria si  dhambi  mwanandoa  yeyote   kuona  kuwa  sasa  hawezi  kuendelea  kuwa  katika  ndoa.  Ni  kwasababu  hii  hata  sheria  ikatambua   uwezekano  wa  watu  kuachana  na  halikadhalika  ikaweka  utaratibu  maalum  kwa  walio  tayari  kwa  hilo.
Tofauti  na kuachana  kwa  mkataba  namna  nyingine  ni  kwa  njia  ya  talaka  mahakamani  na  kwa  njia  ya  kutengana  mahakamani  ambazo  nazo tutaziona  hapa  chini kabla  ya  kutizama  ile  ya  mkataba.

1.KUACHANA  KWA  TALAKA.                                              
Kifungu  cha  99  cha  Sheria  ya  ndoa  kinaongelea  talaka.  Maombi  ya  talaka  hupelekwa  na  yule  anayedhani  hawezi  kuendelea  na  ndoa  kutokana  na  sababu   anazoamini  kuwa ndoa  hiyo haiwezi  kuendelea.  Mahakama  huzisikiliza  pande  zote  mbili  na  kuja  na maamuzi.
Kifungu  cha  107( 2 )  cha  sheria  ya  ndoa  kinazitaja  sababu  ambazo  zote  au  mojawapo  ikithibitishwa  ni  ushahidi  kuwa  ndoa  hiyo  haiwezi  kuendelea.  Baadhi  ni  ukatili, zinaa, kutelekeza, kifungo  cha  maisha  au  kifungo  kisichopungua  miaka mitano,   na  nyingine  nyingi.
Talaka  huombwa  mahakamani  na  hivyo maombi  yake hupelekwa  mahakamani.

2.   KUTENGANA   MAHAKAMANI   BILA  TALAKA.    
Hatua  hii  ni  kwa  mujibu wa  kifungu  cha  99  cha  sheria  ya  ndoa.  Mnatengana  kwa  muda  fulani  lakini  bila  talaka. Talaka  ni  kutengana  milele  wakati  hii  ni  kutengana  kwa  muda.  Njia  hii  nayo   muombaji  hutakiwa  kwenda  mahakamani  na  kufungua  maombi.

Wahusika  wote  wataitwa  na  kila  mmoja  atajieleza na baadae mahakama  itatoa  maamuzi.  Njia  hizi  zote mbili mwombaji  hutakiwa  kupitia  mahakamani  isipokuwa  hii   ya  mkataba  ambayo   itaelezwa  hapa  chini.

No comments: