Saturday, March 4, 2017

SHEREHE YA KUUAGA MWAKA 2016 NA KUUKARIBISHA MWAKA 2017 PAMOJA NA KUAGA WASTAAFU WA JESHI LA POLISI SHINYANGA




Hapa ni ndani ya ukumbi wa NSSF Mjini Shinyanga ambapo usiku wa Ijumaa Machi 3,2017 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanya sherehe ya kuuaga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 pamoja na kuwaaga wastaafu wa jeshi la polisi. 

Mgeni rasmi katika sherehe hizo ambazo zimehudhuriwa na maafisa wa polisi,wakaguzi,askari wa vyeo mbalimbali na wadau wa usalama alikuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga mheshimiwa Zainab Telack. 

Akizungumza wakati wa sherehe hizo Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro alisema Machi 3 kila mwaka huwa ni siku ya Polisi ‘Police Family Day’ ambapo pamoja na kuadhimisha siku hiyo,jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limeamua kuwafanyia sherehe ya kuwaaga wastaafu 10 wa jeshi hilo sambamba na kuuaga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017. 

“Tumeanza sherehe hizi kwa mkuu wa mkoa kukagua gwaride katika uwanja wa Shycom lakini pia kutoa tuzo kwa askari na wadau waliofanya kazi vyema mwaka 2016 katika ulinzi na usalama wa mkoa wa Shinyanga”,alisema kamanda Muliro. 

Naye Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Zainab Telack alitumia fursa hiyo kulipongeza jeshi la polisi mkoani humo kwa kuendelea kuimarisha hali ya ulinzi na usalama na sasa vitendo vya mauaji ya vikongwe na watu wenye ualbino yamepungua kwa kiasi kikubwa. 

Mwandishi wetu,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa sherehe hizo ametusogezea picha 65 za matukio yaliyojiri ukumbini 
Ijumaa Machi 3,2016 katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga-Aliyesimama ni Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akizungumza wakati wa kufungua sherehe ya kuwaaga wastaafu wa jeshi la polisi na kuuaga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017.Kulia ni mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack.Kushoto ni mke wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Mama Muliro 
Kamanda Muliro akizungumza wakati wa sherehe hiyo.Wa kwanza kulia ni Wakili wa serikali mkuu mfawidhi Shinyanga Pendo Makondo akifuatiwa na jaji mfawidhi wa mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga Richard Kibela 
Kamanda Muliro akizungumza ukumbini 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akizungumza ukumbini. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwaomba wadau wote wa ulinzi na usalama kuungana na jeshi la polisi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi katika kuimarisha amani ya mkoa wa Shinyanga 
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini 
Wastaafu wakiwa ukumbini 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga akizungumza ukumbini 
Askofu Mkuu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT),Dayosisi ya Shinyanga, Dkt. John Nkola akiwasalimia wageni mbalimbali 
Viongozi wa migodi na benki mkoani Shinyanga wakiwa ukumbini 
Wadau wa ulinzi na usalama wakiwa ukumbini 
Wadau wakiwa ukumbini 
Wastaafu wa jeshi la polisi wakiwa wamekaa ukumbini 
Kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga Gasto Mkono akiwasalimia wadau walioshiriki sherehe hizo.Kushoto ni Afisa Uhamiaji mkoa wa Shinyanga Annamaria Yondani 
Askari wa jeshi la polisi wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini 
Wadau wakiwa ukumbini 
Wafungua Shampen wakijiandaa kufungua shampen 
Zoezi la kufungua shampen likiendelea 
Waandishi wa habari Moshi Ndugulile kutoka Radio Faraja na Frank Mshana wa ITV/Radio One wakiwa ukumbini 
Viongozi wa dini wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea wakati wa sherehe 
Wadau wakiwa ukumbini 
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga wakigonga cheers na meza kuu 
Zoezi la kugonga cheers likiendelea 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro (wa pili kushoto) akifurahia wakati wa kugonga cheers 
Askofu Mkuu wa Kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT),Dayosisi ya Shinyanga, Dkt. John Nkola akigonga cheers na meza kuu 
Zoezi la kugonga cheers 
Wadau wakiwa katika foleni kwenda meza kuu kugonga cheeers 
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Kadama Malunde akigonga cheers na mke wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro 
Wadau wakiwa ukumbini 
Sherehe inaendelea 
Wadau wakiwa ukumbini 
Sherehe inaendelea 
Mke wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akifungua keki iliyoandaliwa kwa ajili ya sherehe ya kuwaaga wastaafu wa jeshi la polisi.Katikati ni kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro.Kushoto ni MC Mama Sabuni 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akiwa ameshikilia kisu kabla ya kukata keki.Wa pili kutoka kulia ni mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo Elias Mwita 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro na mke wake wakijiandaa kukata keki.Wa pili kutoka kulia ni mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe hiyo Elias Mwita 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akitabasamu kabla ya kuanza kuwalisha keki wastaafu wa jeshi la polisi 
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akiendelea na zoezi la kuwalisha keki wastaafu wa jeshi la polisi 
Tunafuatilia kinachoendelea...... 


Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akiwalisha kesi askari polisi na wadau waliofanya vizuri mwaka 2016 katika kuimarisha ulinzi na usalama mkoani Shinyanga 




Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akimlisha keki mke wake 




Mke wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akila keki 




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack,Jaji mfawidhi wa mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga Richard Kibela(katikati) na Wakili wa serikali mkuu mfawidhi Shinyanga Pendo Makondo (kulia) wakifurahia jambo ukumbini wakati kamanda Muliro akimlisha keki mke wake 




Mke wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga akikabishi keki kwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack kwa ajili ya meza kuu 




Wadau wakiwa ukumbini 




Sherehe inaendelea 




Wadau wakiwa ukumbini 




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akikabidhi zawadi kwa mmoja wa wastaafu wa jeshi la polisi 




Zoezi la kukabidhi zawadi kwa wastaafu wa jeshi la polisi linaendelea 




Zawadi zikiendelea kutolewa 




Mstaafu akishikana mkono na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack 




Wadau wakiwa ukumbini 




Sherehe inaendelea 




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akiwapa zawadi wastaafu wa jeshi la polisi 




Meza kuu wakiungana na mkuu wa mkoa wa Shinyanga kuwapa zawadi wastaafu wa jeshi la polisi 




Utoaji zawadi unaendelea 




Wadau wakiwa ukumbini 




Wadau wakitoa zawadi kwa wastaafu wa jeshi la polisi 




Askari wa kikosi cha usalama barabarani wakipiga picha ya pamoja na mstaafu wa jeshi la polisi Anthony Gwandu (aliyekaa kulia) 




Askari polisi wa kikosi cha usalama barabarani wakifurahia ukumbini 




Kamati ya maandalizi ya sherehe wakijitambulisha ukumbini 




Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Zainab Telack akifungua muziki wakati wa sherehe 




Ufunguzi wa muziki unaendelea 




Wadau wakicheza muziki ukumbini 




Meza kuu na wadau wakicheza muziki ukumbini 




Muziki unaendelea 



Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

No comments: