Saturday, March 4, 2017

JAFFO AZITAKA HALMASHAURI NCHINI KUCHAPA KAZI KWA BIDII

Mkuu wa wilaya ya Longido mkoa wa Arusha,Godfrey Chongolo akizungumza wakati wa zira ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo(kulia)anayesikiliza kwa makini na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa halamshauri ya Longido,Juma Mhina. 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo(kushoto)akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu mkoa wa Arusha,Lootha Laizer 
Baadhi ya Madiwani na watumishi wa halmashauri ya Longido wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo 
Baadhi ya Madiwani na watumishi wa halmashauri ya Longido wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo 
Naibu Waziri Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo(kulia)akizungumza jambo alipotembelea eneo linapojengwa soko la kisasa la mifugo katika Kijiji cha Orendeke Kata ya Namanga mkoa wa Arusha,kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Longido,Godfrey Chongolo. 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo akizungumza na wananchi wa Kata ya Makuyuni wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha baada ya kukagua ujenzi wa Kituo cha Afya,serikali imetenga kiasi cha Sh 700 milioni kwaajili ya upanuzi wa Kituo cha Afya Mto wa Mbu. 
Muuguzi katika Kituo cha Afya cha Usa River,Emiliana Sulle(kushoto) na Mganga Mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Meru mkoa wa Arusha,Bonifas Ukio(kulia)Mh.Suleiman Jaffo kumpima uzito mtoto ili kujua maendeleo yake. 
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo(kulia)akiagana na Mbunge wa jimbo la Monduli,Julius Kalanga baada ya kumaliza ziara yake mkoani Arusha. 


Mwandishi wetu,Arusha

Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi),Mh.Suleiman Jaffo amewataka watumishi katika halmashauri zote nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wawe wabunifu katika kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Katika ziara yake mkoani Arusha katika halmashauri za Meru,Longido na Monduli alisema serikali imeshatoa fedha za Mfuko wa Pamoja wa Afya(Basket Fund)katika halmashauri hizo hivyo kukosekana kwa madawa na vifaa tiba sio jambo linaloweza kuvumilika.

Alisema miradi yote ambayo fedha zimeshaletwa na serikali kuu kwenye halmashauri itekelezwe mara moja ili iweze kuwahudumia wananchi.

No comments: