Sunday, March 5, 2017

AFISA MAENDELEO JIJI LA TANGA AFUNGUA KONGAMANO LA WANAWAKE LA JIJIN HILO AWATAKA KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI KUJIPATIA MAENDELEO

 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga,Mwatumu Dossi akifungua kongamano la Wanawake Jijini Tanga ambalo lilikuwa na lengo kuu la kujadili masuala mbalimbali ya kiuchumi kwa wanawake ikiwemo fursa za kiuchumi sambamba na kupambana na dawa za kulevya kwa jamii lililofanyika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tanga leo
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga,Mwatumu Dossi  wa pili kutoka kulia akiteta jambo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tree of Hope ya Jijini Tanga, Fortunata Manyeresa wakati wa kongamano la wanawake Jijini Tanga kuelekea siku ya wanawake dunia kushoto ni Rehema na Yahaya Seumbe ambaye ni Afisa kutoka Ofisi ya Maendeleo ya Jamii kwenye Jiji la Tanga wakifuatilia kongamano hilo.
 Baadhi ya Wakina wanawake jijini Tanga  wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye kongamano hilo
 Sehemu ya Umati wa wanawake wakifuatilia kwa umakini kongamano hilo la wanawake wa Jiji la Tanga kuelekea siku ya wanawake Dunia ambapo kilele chake itakuwa ni Machi 8 mwaka huu
 Baadhi ya waandishi wa habari jijini Tanga wakifuatilia kwa umakini kongamano hilo wa kwanza kulia ni Burhan Yakub wa gazeti la Mwananchi,Bertha Mwambele wa TBC TV na Sussan Uhinga wa Clous TV
 Sehemu ya wakina wanawake Jijini Tanga wakifuatilia kwa umakini kongamano la wanawake kuelekea siku ya wanawake ambapo kilele chake ni Machi 8 mwaka huu
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga,Mwatumu Dossi akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Dunia Machi 8 mwaka huu mara baada ya kufungua kongamano la wanawake Jijini Tanga.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tree of Hope ya Jijini Tanga, Fortunata Manyeresa akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga baada ya kumalizika kwa kongamano hilo ambapo alisema kuelekea siku ya wanawake kutafanyika shughuli mbalimbali za kijamii
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: