Thursday, February 9, 2017

RAIS SHEIN AONGOZA SHEREHE ZA KILELE CHA SIKU YA SHERIA ZANZIBAR

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifuatana na Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu (kushoto) mara alipowasili katika viwanja vya ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja leo katika sherehe za Siku ya Sheria Zanzibar.
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizindua kitabu cha Sheria ya Mwaka 2015 katika sherehe za Siku ya Sheria Zanzibar zilizofanyika leo katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja,(kushoto) Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (wa pili kulia) akinyanyua kitabu cha Sheria ya Mwaka 2015 baada ya kukizindua   rasmi leo katika sherehe za Siku ya Sheria Zanzibar zilizofanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja,(kulia) Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora (kushoto) makamo wa Pili wa Rais balozi Seif Ali Iddi akifuatiwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake kwa Majaji,Mahakimu na wafanyakazi wakati wa sherehe za Siku ya Sheria Zanzibar zilizofanyika leo katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja,ambapo ujumbe wa mwaka huu unasema "SIMAMIA SHERIA NA MAADILI KATIKA UTENDAJI HAKI" (Picha na Ikulu).
  Baadhi ya Mahakimu na wafanyakazi wa idara ya Maahakama Zanzibar wakiwa katika sherehe ya kilele cha Siku ya Sheria Zanzibar zilizofanyika leo katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja,mgeni rasmi akiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)
 Baadhi ya Viongozi mbali mbali waliohudhuria katika sherehe ya kilele cha Siku ya Sheria Zanzibar zilizofanyika leo katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi  Mnazi mmoja Mjini Unguja,akiwepo jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania Mohamed Chande Othman (wa pili kulia)

No comments: