Tuesday, February 28, 2017

HALMASHAURI YA KAKONKO SHULE ZA KATA ZANG’ARA MATOKEO KIDATO CHA NNE

Lusubilo Joel Ded Kakonko
Na Judith Mhina –MAELEZO
Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko yafaulisha wanafunzi 743 kati ya watahiniwa 784 na kushika nafasi ya Tatu Kitaifa kati ya Halmashauri 178hapaTanzania.
Katika mahojiano maalum na Idara ya Habari MAELEZO Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko Bw Lusubilo Joel Mwakabibi amesema: “Shule za serikali zimeanza kurudisha heshima ya kufaulu kama ilivyokuwa miaka ya 1970 na 1980, mara baada ya matokeo ya kidato cha Nne mapema mwezi huu”.
Mwakabibi ameeleza kuwa Halmashauri hiyo inajumla ya shule           za sekondari 14, kati ya hizo 11 ni za Serikali na 3   za binafsi. Matokeo ya kidato cha nne mwaka huu
Yanaonesha daraja  la  kwanza shule za binafsi ni 10,  pili  35, tatu 40, nne 41 na zilizopata ziro ni 13. Kwa upande wa Shule za Serikali daraja la kwanza 6, pili 47, tatu 149, nne 400 na ziro 38.
 “Siri ya mafanikio yetu ni usimamizi wa karibu na ufuatiliaji shuleni, umoja na mshikamano kati ya Walimu, wazazi, Viongozi wa Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa wilaya; walimu wetu tupo pamoja nao, tunawatia moyo katika kazi ya kufundisha”. Anafafanua Mkurugenzi huyo.
Aidha, Mkurugenzi Mwakabibi amesema mwaka 2016 Halmashauri imeshika na fasiyatatu, Kitaifa katika Halmashauri 178 Tanzania, kwani matokeo ya kidato cha Nne na Pili mwaka 2015, Halmashauri yetu, ilikuwa ya kwanza kitaifa na kuzawadiwa ngao ya ushindi toka Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia. Hata hivyo ameeleza kuwa mikakati ya Halmashauri yake ni kurudi namba moja, lengo likiwa ni kuhakikisha wanafunzi wote watakao sajiliwa kufanya mtihani wa kufaulu kwa viwango vya juu na kufuta kabisa aibu ya kufeli..
Bw Mwakabibi amesema kati ya watahiniwa 794 wa Kidato cha Nne 743 wamefaulu na wanafunzi 51 tu ndio waliofeli. Shule ambayo imeongoza matokeo ya kidato cha nne ni ya binafsi ya Mtakatifu Thomas More Kibogora iliyotahini wanafunzi 30, mbili za binafsi matokeo yake ya kosa wana shule zetu za serikali na idadi ya wanafunzi ni 55.  Huu niuthibitisho dhahiri kuwa shule za Sekondari za Serikali zenye watahiniwa 709 ambazo ni Kata zimefanya vizuri kama shule za binafsi.
Kuhusu masomo waliyofaulu, Mwakabibi amesema kuwa watahiniwa wamefanya vizuri zaidi katika masomo ya Uraia (Civics), Historia, Biolojia, Kingereza, Jiografia, na Kiswahili na kubainisha kuwa ufaulu ni matokeo ya uwepo wa walimu wakutosha na wenye uwezo mkubwa wa ufundishaji na kufanya kazi kwa bidii na kujituma
“Ili tuendelee kuwa namba moja, Halmashauri inasimamia walimu katika kazi zao, inawahudumia na kujali mahitaji yao.  Pia, inashirikiana na shule, wazazi, wadau wengine iliwanafunzi wajifunze kwa bidii na vitendo iliwapate maarifa na kutumia elimu yao katika maisha ya kila siku, vilevile halmashauri ipate matokeo bora zaidi”. Amesema Mwakabibi
Mwakabibi alisisitiza kuwa “Mafanikio yetu ya mechangiwa na wazazi, walimu, Ofisi ya Mkurugenzi, Waheshimiwa Madiwani, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na wadau mbalimbali kama Mpango wa Ubora wa Elimu Tanzania EQUIP-T , kwa kuunda Ushirikiano wa Wazazi na Walimu (Parent Teachers Participation).
“Ushirikiano huu, umesaidia kuwatia hamasa wazazi kushirikiana vizuri na walimu katika zoezi zima la kuchangia chakula, kwa kutoa mahindi kilo tano kila mzazi kwa muhula mmoja”. Alifafanua Mkurugnezi huyo na kuongeza kuwa hatua hiyo imewezesha watoto kuwa na usikivu wakati wa ufundishaji na ujifunzaji  na kuongeza ufaulu”.
Akichangia utoaji wa chakula shuleni Afisa Elimu Sekondari Bw Joseph Mutahaba amesema “Kakonko imefanikiwa kutoa chakula au uji katika shule za Msingi 59 zaserikali”. Huu ni utekelezaji wa agizo la Serikali la wanafunzi kupata chakula wawapo shuleni. Zoezi hili limefanikiwa baada ya kuhamasisha na kuwaelimisha wazazi juu ya umuhimu wa kuchangia chakula au uji kupitia vikao mbalimbali.
Bwana
Mutahab Alitoa Wito kwa Halmashaurinyinginekuhakikishakuwazianakuwana:“Usimamiziwakaribuwataalumashuleni, kuwajali walimu, kuwapa moyo, kuwasikiliza shida zao, kuwahamasisha wafundishe kwa bidii, ushirikiano wa karibu wa wazazi, walimu na wadau wengine wa Elimu katika kuboresha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji” na kusisitiza kuwa “Haya ni mambo ya msingi sana”.
Tofauti na Halmashauri nyingine ambazo zina shule nyingi za binafsi ambazo hunyanyua viwango vya ufaulu wa Halmashauri hizo lakini kwa upande wa  Kakonko ambayo ina idadi ndogo ya shule za binafsi, shule za Serikali zimesaidia kunyanyua kiwango cha ufaulu hadi kushika nafasi ya tatu Kitaifa katika Halmashauri. Ulinganisho huo umefanywa kwa kupata maelezo ya:
Afisa Elimu Mkoa wa Njombe Bw Halfan Omary Masukira amesema: “Halmashauri ya Mji Njombe shule za binafsi zilizotahiniwa 16; daraja la kwanza 58, pili167,tatu 162, nne 168 naziro 12. Shule zaserikalizipo15 daraja la kwanza 11, pili 61,tatu146,nne584 naziro 105 jumlawatahiniwa 1538” 
Afisa Elimu Sekondari Mkoa wa Kagera Bw Wandare Lwakatare amesema: Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba shule za binafsi zilizotahiniwa 13; daraja la kwanza 133, pili 209, tatu 171, nne 188 na ziro 16. Kwa upande wa Shule za serikali ni 16; daraja la kwanza 24, pili 97, tatu 167, nne 550 na ziro 190 jumla watahiniwa 1757. 
Ukiangalia takwimu za Halmashauri hizo tatu utagundua kuwa shule za Kata za Kakonko zimefanya vizuri kuliko za Kata za Halmashauri ya kwanza na ya pili.  Halmashauri ya kwanza Tanzania katika ufaulu wakidato cha nne ni Manispaa ya Bukoba; kati yawatahiniwa 1757 waliofaulu ni 1542, waliofeli 215 na kupata GPA ya 3. 5414 ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe ambayo ilikuwa na watahiniwa 1538 na walifaulu 1418, waliofeli 120 na kupata GPA 3.6453. Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko ndio iliyoshika nafasi ya tatu ambayo ilikuwa na watahiniwa 794 kati yao watahiniwa waliofaulu ni 743 na waliofeli ni 51 na kupata GPA ya 3.6716. Kakonko ndio Halmashauri yenye wanafunzi watahiniwa wachache zaidi katika Halmashauri kumi bora.
New Picture

No comments: