Wednesday, February 22, 2017

DKT. KALEMANI AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MIRADI JIMBONI KWAKE



Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (aliyevaa miwani) akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nyakayondo kuhusiana na utekelezaji wa miradi mbalimbali kijijini humo na jimboni kwa ujumla.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akielekeza jambo wakati wa ukaguzi wa kisima (kilichofunikwa kwa nyasi) kilichochimbwa katika kijiji cha Nyakayondo. Jumla ya visima virefu 30 vinatarajiwa kuchimbwa jimboni humo.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi ya Nyarututu, iliyopo Kata ya Bwanga. Jumla ya vyumba vya madarasa vitano na matundu 30 ya vyoo vinatarajiwa kujengwa katika shule hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (katikati) akiongozana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Chato, Ibrahim Bagula (kushoto) na Diwani wa Kata ya Bwanga, Nuhu Mahmoud (kulia) wakati wa ukaguzi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa Jimboni humo.

Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (kushoto) akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Chato, Shaban Ntalambe (kulia) na Diwani wa kata ya Bwanga, Nuhu Mahmoud (katikati) wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na ofisi ya walimu katika shule ya Msingi ya Bwanga B. Mradi huo unahusisha ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa, ofisi ya walimu na matundu 30 ya vyoo.
Mbunge wa Jimbo la Chato na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (wa pili kushoto) akielekeza jambo wakati wa ukaguzi wa utekelezaji wa miradi mbalimbali jimboni humo. Kulia ni Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Chato, Mhandisi Mali Misango. Nyuma ya Dkt. Kalemani ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chato, Christian Manunga.

No comments: