Saturday, December 24, 2016

Yaliyojiri Katika Vituo Mbalimbali vya Televisheni

SIMU TV: Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro amesema watu wawili wameuawa kwa kupigwa risasi wakati wa msako wa waharifu; https://youtu.be/9j9MxtuOOqE

TBC: Jeshi la polisi limekamata zaidi ya magunia miambili ya mkaa yaliyokuwa yakisafirishwa kwenda Mwanza kinyemela; https://youtu.be/EkwsUh1w_Ak

SIMU TV: Mkuu wa wilaya ya Hai amewakamata na kuwaweka ndani maafisa wawili wa ushirika kwa kushindwa kutekeleza agazo alilowapa; https://youtu.be/8saJQ2iRZZA

SIMU TV: Waziri wa ardhi William Lukuvi aziagiza halmashauri kanda ya kaskazini kusimamia na kulinda maeneo wanayoishi kabila la Wahadzabe; https://youtu.be/DxpnU1NPYkQ

TBC: Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu awataka wananchi Zanzibar kuzitumia Madrasa katika malengo yaliyokusudiwa; https://youtu.be/kkvHFB4ayhA

SIMU TV: Watu wawili wafariki dunia na wengine kulazwa kutokana na kulipuka kwa ugonjwa wa Kipindupindu mkoani Dodoma; https://youtu.be/4rmhl8dZgfg

SIMU TV: Mamlaka ya udhibiti wa nishati na maji EWURA yawasilisha mapendekezo ya bei elekezi ya gesi asilia; https://youtu.be/tTL_eC2J50c

SIMU TV: Mjasirimali Rukia mkazi wa Kijitonyama Dar es Salaam awataka wajasiriamali kuwa wabunifu katika biashara zao; https://youtu.be/i3wKwCf5ar8

SIMU TV: Timu ya Yanga yabanwa mbavu kwa kutoa sare ya goli moja kwa moja na timu ya African Lyon katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara; https://youtu.be/7XJGrUvzuuM

SIMU TV: Timu ya Simba kesho itashuka katika dimba la Uhuru kukipiga na timu ya JKT Ruvu katika mchezo wa ligi kuu soka Tanzania bara; https://youtu.be/hsvr8C1aKeY

SIMU TV: Mkuu wa wilaya ya Ilala Sophia Mjema awataka wananchi kupenda kushiriki katika michezo ya bahati nasibu; https://youtu.be/yrcGZ83FjUU

SIMU TV: Msaani wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz anatarajia kutumbuiza mkoani Iringa Disemba 25 mwaka huu; https://youtu.be/3uwpCwMRK94

SIMU TV: Rais Dkt John Magufuli amemuapisha Jaji Semistocles Kaijage kuwa mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi NEC ; https://youtu.be/6WuBDqTy_AI

SIMU TV:  Rais Dkt John Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wamemtembelea na kumjulia hali Kadinali Pengo ambae amefiwa na dada yake; https://youtu.be/GE7OFyeM74c

SIMU TV:  Mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Jaji Semistocles Kaijage amesema chaguzi zote ndogo zitafanyika January 22. 2017 ; https://youtu.be/TKRA9mlTqbU

SIMU TV:  Kukithiri kwa uharibifu wa mazao unaofanywa na wanyama pamoja na ukame wa kudumu vimetajwa kuwa ni sababu za kuzuka kwa njaa Mara; https://youtu.be/soYW6Eer35Q

SIMU TV:  Vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa watoto na wanawake vimezidi kuathiri maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi wilayani Karatu; https://youtu.be/iRXrwGqr6Tc

SIMU TV:  Chama cha watu wenye Ualbino leo kimeikumbusha serikali kuwaharakishia upatikanaji wa Bima kwa ajili ya kutunza afya zao; https://youtu.be/GsV7gnV9sIQ

SIMU TV:  Serikali imeombwa kupunguza baadhi ya kodi kwa bidhaa zinazozalishwa ndani ili ziweze kushindana na zile zinazoingizwa kutoka nje; https://youtu.be/O29kWYfqkDI

SIMU TV:  Mamlaka ya udhibiti wa nishati na maji EWURA imekutana na wadau wa nishati ya gesi nchini ili kujadili bei ya elekezi ya gesi; https://youtu.be/a4hPPCksCCE


SIMU TV:  Klabu ya soka ya Stand United imesema licha ya kupoteza mchezo wao wa kwanza bado akili zao wamezielekeza kwa Kagera Sugar; https://youtu.be/fn7-RxrPNwI

SIMU TV:  Kocha mkuu wa klabu ya Azam amesema timu yake itafanikiwa kutinga katika hatua ya makundi baada ya kufanya mazoezi ya nguvu; https://youtu.be/1Oaiq0Xbyaw

SIMU TV:  Timu ya taifa ya Senegal imefanikiwa kuwa kinara katika viwango vya soka duniani baada ya kushika nafasi ya 33 kidunia na namba moja Afrika; https://youtu.be/Klk9gU3CSRs

No comments: