Friday, December 23, 2016

TAASISI YA UTAFITI YA MAGONJWA YA BINADAMU KILIMANJARO (KCRI) YAWAKUMBUKA WATOTO WANAOLELEWA KITUO CHA UPENDO NA WALIOLAZWA KCMC.

Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) wakiwa katika picha ya pamoja na zawadi walizopeleka katika kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Upendo cha mjini Moshi.
Zawadi ya Kei iliyotolewa kwa watoto wa kituo cha Upendo cha mjini Moshi.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro,(KCRI) Profesa Blandina Mbaga akisalimiana na Msimamizi wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Upendo cha mjini Moshi Sister Yasinta walipofika kwa ajili ya kutoa zawadi kwa watoto wa kituo hicho.
Msimamizi wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Upendo cha mjini Moshi,Sister Yasinta Diwi akiwaeleza historia ya kituo hicho wafanyakazi wa taasisi ya utafiti ya magonjwa ya binadamu Kilimanjaro (KCRI).
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) Prof Blandina Mbaga akizungumza na Mkurugenzi wa fedha Hosptali ya Rufaa ya KCMC,Hilda Mungure (katikati) na Elizabeth Msoka.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) wakiwa wamebea zawadi kwa ajili ya watoto wa kituo cha Upendo cha mjini Moshi.
Msimamizi wa Kituo cha Upendo cha mjini Moshi ,Sista Yasinta Diwi akiwaongoza watoto wanaolelewa katika kituo hicho kuwaimbia wageni waliofika katika kituo hicho kwa ajili ya kutoa zawadi. 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) akitoa zawadi kwa watoto wa kituo hicho. 
Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) wakifurahia na watoto wanaolelewa katika kituo cha Upendo cha mjini Moshi.
Mfanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) Anita akiwapa vipande vya Keki watoto wanaolelewa katika kituo cha Upendo cha mjini Moshi.
Mtoto Mwenye Umri wa wiki tatu anayelelewa katika kituo cha watoto cha Upendo baada ya kupelekwa kituoni hapo kufuatia mama wa mtoto huyo kuwa na ugonjwa wa akili. 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) Prof Blandina Mbaga akizungumza muda mchache kabla ya kuwaona watoto waliolazwa katika Hosptali ya Rufaa ya KCMC.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) wakitoa zawadi kwa watoto waliolazwa katika wodi za watoto Hosptali ya Rufaa ya KCMC.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu Kilimanjaro (KCRI) wakirejea mara baada ya kutoa zawadi katika kituo cha Upendo na watoto waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

No comments: