Friday, December 9, 2016

MKUU WA MKOA AMALIZA MGOGORO WA MAJI – MAKILENGA

Mkuu Wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (katikati) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Alexander Mnyeti(kushoto0 wakiwalia katika kijiji cha Nkoasenga kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa maji Makilenga.
Mhandi wa Maji Happy Mrisho (aliyesimama) akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha(hayupo pichani) wakati wa kikao cha kutafuta ufumbuzi wa mgogoro wa Maji Makilenga.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Makilenga waliohudhuiria kwenye Mkutano wa hadhara.
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alaxander Mnyeti akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nkoasenga kwenye Mkutano wa hadara.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo (aliyesimama mbele) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nkoasenga kwenye Mkutano wa hadhara
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Nkoasenga wakifurahia makubaliano yaliyofikiwa katika ya Serikali na kijiji hicho ya kulipa Tsh 1500 kwa huduma ya maji mwezi mzima kwa wanaotumia mabomba ya Kijiji .


Nteghenjwa Hosseah – Arumeru


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe . Mrisho Mashaka Gambo amemaliza mgogoro wa muda mrefu uliodumu zaidi ya miaka mitatu kati ya Bodi ya Maji ya Makilenga na wananchi wa Kijiji cha Nkoasenga, Kata ya Leburuki Wilayani Arumeru. 

Utatuzi wa mgogoro huo ulifikiwa kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Kijiji cha Nkoasenga baada ya Mhe. Gambo kuwashirkisha wananchi wa aneo hilo katika kutatua changamoto hii iliyoathiri wananchi zaidi ya hamsini elfu wa kijiji hiki pamoja na vijiji vingine ishirini na sita vinavyotegemea mradi huo.

Wananchi hawa waliofungiwa maji kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa baada ya kufanya uharibifu wa miundombinu ya Maji pamoja na kuweka kinyesi kwenye mabomba walionyesha kuchoshwa na adha hiyo ya kufuata maji umbali mrefu na kwa gharama kubwa zaidi ilihali maji yanapatikana katika Kijiji chao na walionyesha hali ya kutaka muafaka wa jambo hili ili kuendelea kupata huduma ya maji kama ilivyokuwa hapo awali.

Akiongea katika Mkutano huo baada ya mazungumzo na viongozi wa Kijiji pamoja wananchi Mkuu wa Mkoa Mhe. Mrisho Gambo alisema katika kutoa huduma ya Maji Vijijini tunaongozwa na Sera ya Maji ya mwaka 2002 inayotaka kuchangia hudma za maji na sio kununu Maji hivyo kila kaya inawajibu wa kuchangia kiasi kidogo cha Fedha ili kuwezesha huduma hii iendelee kutolewa siku zote.

“Tunafahamu kwamba maji haya yanaanzia kwenye Kijiji hiki na wakazi wa Nkoasenga ndio walinzi wakuu wa mradi huu na wanastahili kupewa upendeleo wapekee katika kutumia maji haya ili wendelee kutunza mradi huu wa Maji, ni wazi kuwa vijiji vya ukanda wa chini haviwezi kupata Maji endapo tu wana Nkoasenga wataharibu mradi huu wa maji mtiririko”, Alisema Mhe. Gambo.

Aliongeza kuwa umuhimu huu wa nyie kuwa Kijiji mama cha mradi huu hauwapi Kinga ya kutokuchangia gharama za maji, hivyo nataka mniambia mnaweza kuchangia kiasi gani kadiri ya uwezo wenu na baada ya makubalino haya mtalipia gharama za maji kwa mwezi na sio kwa mwaka tena kama mlivyokuwa mnafanya hapo awali”.

Awali akizungumza katika Mkutano huo Mhandisi wa Maji Bi. Happy Mrisho alisema “mradi wa maji Makilenga uliibuliwa na wananchi wa Kijiji cha Nkoasenga na baada ya thatmini ya awali ilonekana kuwa mradi ni wa gharama kubwa hivyo usingekidhi vigezo vya kiufadhili kama ungekua mradi wa kijiji kimoja na ili kukidhi vigezo vya kupata fedha toka kwa wafadhili ililazimu kuongeza wanufaika kutoka vijiji 26 na utekelezaji ukaendelea”.

Aliongeza kuwa baada ya mradi kukamilika iliundwa Kamati tendaji ya Makilema ambayo ndiyo inayosimamia mrdai huu na Madiwani na wenyeviti wote wa vijiji waliingia makubaliano ya kuchangia Tsh 10 kwa ndoo lakini baada ya muda mfupi wanakijiji wa Nkoasenga walikiuka makubalino hayo na kudai watalipa Tsh 5000 kwa mwaka na hawewezi kulipa kwa ndoo kwa kuwa maji hayo ni mali ya Kijiji.

Anderson Sikawa ni Diwani wa Kata ya Leburuki kilipo kijiji cha Nkoasenga alisema hawakatai kuchangia huduma za Maji lakini kutokana na hali duni ya wananchi wa eneo hilo hawawezi kulipa kwa ndoo hivyo wanahitaji kufanya mapitio ya gharama za Maji ili kuendana na hali ya wana Nkoasenga ambayo pia itawaongezea ari wakazi hao kulinda mradi huo kwa manufaa ya vijiji vingine pia alitoa tuhuma kwa Bodi ya Makilenga kwa matumizi mabaya ya Fedha za maji.

Katika kutoa mapendekezo ya kiasi stahiki cha kuchangia huduma ya Maji Ndg. Afred Masao ambaye ni mwananchi wa Kijiji cha Nkoasenga aliwakilisha wananchi wote wa Kijiji hicho alisema kuwa wananchi wako tayari kuchangia kwa mwezi lakini uwezo wao ni Tsh 1500 na sio Ths 3000 kama ilivyopendekezwa kwenye vikao vya ndani katika ya Mkuu wa Mkoa na viongozi wa Kijiji.

Rc Gambo alihitimisha Mkutano huo kwa kukubaliana na mapendekezo ya wananchi kuwa watalipia Tsh 1500 kwa mwezi kwa wale wanaotumia mabomba ya Kijiji na kwa wale wenye mabomba nyumbani watalipia kadiri ya matumizi yao kwa mwezi na wote watafungiwa Mita za Maji pia aliwaagiza wananchi hao kulipia gharama hizo Halmashauri na sio kwa Kamati ya Maji Makilenga kama awali.

Mradi wa Maji wa Makilenga ulianza mwaka 2011 kwa lengo la kutoa huduma ya Maji na kuhudmia Kata nne na vijiji 27; Ulifadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya kwa kutoa kiasi cha Tsh Bil 3.7, OIKOS pamoja na nguvu za wananchi. Mradi huu unaendeshwa na Jumuiya ya watumiaji maji ya Makilenga ambayo ina jukumu na mamlaka ya Kisheria kusimamia mradi huu wa maji.

No comments: