Wednesday, December 14, 2016

HAPI APOKEA MADAWATI 80 KUTOKA KWA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU NCHINI LEO JIJINI DAR ES SALAAM

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi akikata utepe kuashiria upokeaji wa  madawati ya msaada kutoka kwa Wakala wa  Huduma za Misitu nchini leo jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akizungumza mara baada ya kupokea madawati 80 yenye thamani ya shilingi milioni 5.6  kutoka kwa Wakala wa  Huduma za Misitu nchini leo jijini Dar es Salaam. Picha zote na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
Meneja wa Wakala wa Huduma za  Misitu Tanzania Wilaya ya Kinondoni, Alexander Mboya akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kukabidhi madawati kwa mkuu wa Wilaya leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Alli Hapi.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Alli Hapi na Meneja wa Meneja wa wakala wa huduma za  Misitu Tanzania wilaya ya Kinondoni, Alexander Mboya wakiwa wamekaa kwenye madawati mara baada ya kukabidhi leo jijini Dar es Salaam.

No comments: