Wednesday, December 14, 2016

BARUA YA WAZI KWA MUHESHIMIWA RAIS JOHN POMBE MAGUFULI

 Muheshimiwa Rais,
Kwanza kabisa napenda kutoa pongezi na shukran zangu za dhati kabisa, kwa muendelezo na juhudi zako ktk kuweka maslahi ya nchi na wananchi mbele, moja ya juhudi hizo ni ktk harakati zako za usimamiaji wa mapato ya umma na uboreshaji wa utendaji wa wafanyakazi wa mashirika na taasisi za umma, ambapo sehemu moja ya juhudi hizo tumeziona ktk kupambana kidhati ktk kukomesha ulaji rushwa makazini na kuondoa wafanyakazi hewa, hivyo basi kuendeleza ufanisi ktk sekta za serikali na sekta ndogo ndogo za watu binafsi kama mimi na wengine wengi tu, ambao wako ktk mkwamo mzima wa mzunguko wa hela hapa nchini.
Hata hivyo muheshimiwa Rais, kuna malalamiko ndani ya nchi na nje ya nchi hususan kwa wafanyabiashara wadogo wadogo, yaani small na medium enterprise businesses, yaani mifano ya Matonya Enterprises.
Kwanza kabisa, Muheshimiwa Rais, ningependa kukufahamisha profile yangu in general, mimi ni mzawa na maskini ambaye anamudu huduma zake za hapa na pale, nina nyumba mbili, moja ninaishi mwenyewe, na nina duka dogo la kuuza spares za magari.  Nimeajiri wafanyakazi (Direct employment) wanne, na indirect employement, ukiingiza na wafanyakazi wa part time, ninaweza kuwakisia kufikia 10,  ukiingiza Mafundi, Madalali, nk. Ninafanya kazi muda wa masaa 14-16 kwa siku, na mapumziko madogo siku ya Jumapili. Yaani ninaweza kusema nina jitahidi sana ktk kazi yangu.
Sehemu kubwa ya kazi ambayo inanipatia riziki yangu zaidi ya kuuza spares, ni uingizaji wa magari aina ya malori kutoka Europe(UK, Sweden, Japan, nk) kuleta Tanzania, na vile vile ninaweza kusema na kujiproud kuwa ni mlipaji kodi mzuri tu, ambapo malipo yangu ya kodi ni wastani wa takribani Millioni za Kitanzania zisizopungua 180-200 kwa mwaka, kupitia shirika la ukusanyaji kodi la TRA, Customs na ulipaji wa TBS(Vehicle Inspections), lakini hata hivyo Muheshimiwa Rais kuna kitu kinanishughulisha kimawazo na imenifanya niwe na maswali mengi bila majibu ya kuridhisha.
Kabla ya kuuliza hayo maswali yangu, kwanza kabisa nataka nikupe hesabu ndogo kuhusiana na ulipaji kodi ambao ninaufanya ktk sekta yangu ya kibiashara kwa kuweka wazi vikokotoo vya gharama za Kodi ya importation ya unit moja tu ya Lorry kama ifuatavyo :-

Mathalani, Nikiagiza Gari Tanzania aina ya Scania 94D, 6 * 2 ya mwaka 2001(lorry la kubebea mizigo kwenda mikoani) toka dealership ya UK au Sweden.
Tathmimi ya malipo yapo ktk pesa ya kigeni, US$                                                            
 Import Duty                                      $3848.63
Excise Duty                                         $5773.00
VAT                                                        $4605.37
Customs Processing Fee                               $92.37
Railway Dev. Levy                            $230.92
Total Taxes                                         $14550.29

Yaani Malipo yote yanaoingia serikalini ni 31,983,047.03 Tshs, Takribani milioni 32 pesa za kitanzania. Na hapo hapo Muheshimiwa Rais sijaingiza gharama za Agent Fees, TBS certification ambazo ni £150, na gharama nyengine ndogo ndogo.

Muheshimiwa Rais, Gari hio hio ninategemea ikae sokoni, kwa muda wa takribani ya wastani ya miezi 3 mpaka mwaka 1, kwa mustakbali wa hali ya mzunguko wa pesa ulivyokua mdogo kwa hivi sasa, sehemu kubwa ya wateja wangu ni matonya kama mimi, ambao wanategemea mikopo ya bank, retirement funds, ili kujiingiza katika shughuli na sekta ya usafirishaji na wao wapate ugali wao.
Muheshimiwa Rais Hali ngumu sana ya kimaisha, biashara yangu imeathirika na kushuka kwa mauzo ya 50% kwa mwaka huu peke yake, hivi sasa binafsi niko ktk stage ya kuanza kula mtaji wangu, na hivyo kuvunjika kimapato na kushuka kwa ulipaji kodi toka kwangu kuingia serikalini, na hivyo basi hatma yake ni kufa kwa biashara, lakini mimi binafsi na wengine, tunategemea hali itakua nzuri, panapo majaaliwa, Bank zitaanza kukokepesha tena, sector ya usafirishaji binafsi kuanza kukua itakapofika kati kati ya mwaka 2017, tukitegemea makubaliano uliyoingia nayo na nchi ya Congo, na Rwanda hivi karibuni, kuweza kutumia bandari ya Dar.

Baada ya maelezo mafupi ya nini ninafanya kupata riziki yangu, Hoja yangu Muheshimiwa Rais ni kama ifuatavyo!
Nimeona picha za magari za Dangote, kwenye meli ambayo hivi karibuni imetia nanga na kushusha baadhi ya sehemu ya magari 600 siku mbili tu, baada ya kutoa ahadi aliyoitamka Dangote hapo ikulu hii majuzi. Je hii ni calculated move, kukuhadaa wewe na kupata Baraka zako Muheshimiwa Rais kwa upande wa Dangote, ukizingatia kuwa kauli zilizokua zikitolewa na mawaziri husika zilikua ziko tofauti na matamko na steps zilizochukuliwa na Dangote Cement, Mtwara, ie Kufunga Kiwanda kwa muda, nk. Kwa hio alikua anategemea a better deal toka kwako, na kupata Baraka za kuingiza magari chakavu, ndani ya nchi, na vile vile kuzitupilia mbali taratibu za uingizaji wa bidhaa kama magari, kuhakikiwa ubora wake, yaani kupitia TBS, kama ambavyo Matonya Enterprise tunazifuata.
Muheshiwa Rais, kwa kuangalia kwa ukaribu vile vile Magari yaliyoshushwa sio magari mapya, Je TBS walihusishwa katika uhakiki wa ubora wa magari hayo.
Muheshimiwa Rais Suala la pili ambalo ndio muhimu katika yote,  Je Dangote Group, amelipia ushuru kiasi gani  wa hizo gari, au pia alipata Baraka za kuingiza hizi gari kwa ushuru mdogo bila ya uhakiki wa TRA ?
Muheshimiwa Rais, kama nikikokotoa hesabu za ushuru wa kila Lori, mathalani ushuru wa lori moja takribani ni US$10,000 ulinganisha na Scania ambapo hapo juu ni US$14550, kwa hiyo nimefanya mapungufu ya zaidi ya US $4550,   kama malori yote 600 yatalipiwa ni sawa  US $ 6,000,000 sawa na rate ya leo ya wastani wa 2200 per US $ 1, kwa hiyo Jumla ya kodi anayotakiwa kulipa Dangote Group  kwa uingizaji ya magari hayo ni Bilioni 13.2 TZShs, Je hizi pesa zimelipwa, kama tunavyolipa cash sisi Matonya Enterprise,  Je TBS imelipwa kama inavyostahiki, takribani £150 *600 = UK £90,000 ni  Milioni 252 Tzshs,
Ningependa sana Muheshimiwa Rais na taasisi husika kutujibu maswali yetu hapo juu na kupatia vielelezo vya taratibu nzima, zilizoihusisha idara zote, katika uingizaji wa magari 600, ie TBS, TRA, TPA na Customs Office.
Na Suala la mwisho, Muheshimiwa Rais, Kuhusiana na Dili la kununua Gesi moja kwa moja kutoka kwenye shirika la uzalishaji Gesi kwa bei ndogo kabisa, Je mashirika mengine ya Matonya Enterprises, Cements Companies, pamoja na mashirika makubwa ya binafsi kama Azam na mengineyo, wataruhusiwa kupewa Gesi ktk bei hiyo hiyo aliyopatiwa Dangote na kukata dearliship ya mtu wa kati ?,
Malalamiko yetu, Muheshimiwa Rais sisi wafanyabiashara wadogo wadogo, tumekua tukisumbuliwa mara kwa mara na TRA, kuhakiki ulipaji wa kodi, ukizingatia kwamba, malipo yetu yako wazi kupitia bidhaa tunazoziingiza through customs, kodi hizi ambazo zinaongezeka mara kwa mara bila ya kutolewa proper notice, mathalani kodi ya kuingiza lori aina ya Scania 94D, mwaka jana peke yake imeongezeka zaidi ya mara moja, Muheshimiwa rais kodi tunazolipa si bidhaa ndogo ndogo ni kodi ambazo haziwezi kufichika, na vile vile tunafanya malipo ya VAT na filling ya Income Tax ya kila mwaka.
Muheshimiwa Rais, Naomba uzingatie kwamba, wateja wetu ni wafanyabiashara wadogo wadogo, haya maongezeko ya kodi, yanaathiri biashara zao, na yanaathiri ujumla wa ulipaji wa kodi kutoka sehemu kubwa ya wafanyabiashara wadogo wadogo ambao ndio msingi wa uendelezaji wa nchi kupitia malipo ya kodi, yanayofanyika mara kwa mara.

Kumbuka kwamba mimi Matonya Enterprise tunalipa kodi kubwa in average ya Milioni 180-200 pesa za kitanzania kwa mwaka.

Mwisho kabisa, napenda kukushukuru Muheshimiwa Rais kuisoma barua hii,
Mungu ibariki Tanzania na watu wake!
Hapa Kazi tu!
Kidumu Chama Cha Mapinduzi!
Andrew M!


No comments: