Tuesday, December 6, 2016

Airtel yaungana na Umoja Switch kutoa huduma za kifedha kupitia simu

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imeshirikiana na  UMOJA SWITCH ATMS katika kuwawezesha wateja wake wa Airtel Money kufurahia huduma za kifedha na kutoa pesa kwenye mashine za ATM za UMOJA SWITCH nchi nzima bila kuwa na kadi ya ATM. 
Ushirikiano huu mpya utasaidia kurahisisha huduma za kifedha kwa watanzania na kuwawezesha kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa ufanisi zaidi, wateja wa Airtel sasa wanaweza kupata huduma za kifedha wakati wowote masaa 24 siku 7 za wiki kupitia mashine za UMOJA SWITCH ATMs zilizoendea nchi nzima
ushirikiano huu pia utasaidia  katika kutanua wigo wa mawakala wa Airtel Money ambapo wateja wa Airtel hawatakuwa na haja ya kufungua akaunti ya benki wala kuwa na ya kadi ya ATM ili kupata huduma hii, kwa kupitia mashine za UMOJA SWITCH ATMs mteja ataweza kufanya muamala kutoka kwenye simu yake ya mkononi na maramoja kutoa pesa zake kwenye mashine ya ATM kwa gharama nafuu. Kiwango kidogo kitatozwa kama tozo kulingana na kiasi cha pesa ambacho mteja atatoa.
Akiongea wakati wa uzinduzi, Meneja kitengo cha Airtel Money, Moses Alphonce alisema” kupitia huduma yetu ya Airtel money tunaendelea kutumia technologia ya kisasa katika kuhakikisha tunatoa huduma bora zinazotoa suluhusho na kutatua changamoto katika huduma za kifedha kwa wateja wetu. 
Ushirikiano huu kati ya Airtel na Umoja SWITCH utaleta ufanisi na urahisi katika huduma zakifedha kupitia simu za mkononi”
Kupitia ushirikiano huu pia tunaongeza idadi ya mawakala ambao kwasasa ni zaidi ya mawakala 85,000 nchini nzima,sasa wateja wetu wanauhakika wakupata pesa kupitia mashine za ATM za Umoja SWITCH wakati wowote.
Lengo letu ni kuhakikisha tunaongeza idadi ya mawakala kwa kupitia njia mbalimbali na kuhakikisha huduma za kifedha kupitia simu za mkononi zinapenya na kuwafikia watanzania wengi na hivyo kuleta tija katika shughuli zao za kiuchumi na kijamii kwa ujumla. Aliongeza Alphonce
 Kwa upande wake  Afisa Mtendaji Mkuu wa Umojaswitch, Danford Mbillinyi alisema”  kuingia kwa makubaliano katika huduma ya Airtel Money kuthihirisha lengo letu la kuchochea ushirikiano wamakapuni katika huduma za kifedha nchini. 
Tumekuwa ni sehemu ya Airtel katika huduma inayomuwezesha mteja kutoa pesa benki kwenda Airtel Money na Airtel Money kwenda benki na sasa tunafungua milango mingine kwa wateja wa Airtel Money kutoa pesa katika ATM zetu kwa urahisi na uhakika  kwa kutembelea katika ATM zetu nchi nzima. 
Alisisitiza Umojaswitch iko tayari kuungana na makampuni yanayoamini katika ushirikiano wa kibiashara kwani tunatambua kwa kufanya hivyo kutaleta tija kwa wateja na uchumi wananchi” 
Ili kupa huduma hii , mteja atatakiwa kupiga *150*60# kupitia simu yake ya mkononi  kisha kuchagua kutoa pesa kupitia ATM, kisha kuchagua UMOJA SWITCH ATM   na kupata namba maalumu ya kwaajili ya kutoa pesa.  Namba hiyo itatumika katika kutoa pesa kwenye mashine yoyote ya ATM ya UMOJA SWITCH Tanzania. Kila token (namba) itakayotolewa itatumika mara moja na itadumu kwa muda wa dakika tatu (3)


No comments: