Wednesday, November 16, 2016

THBUB YASHUKURU UN KWA KUSAIDIA PROGRAMU ZA SHERIA

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeshukuru Umoja wa Mataifa kwa msaada wake mkubwa inaotoa kwa taasisi zisizo za kiserikali za kujengea uwezo wa kuweza kutetea haki za binadamu nchini Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay wakati wajumbe wa nchi za Nordic ambao ni wafadhili wakubwa wa programu za Umoja wa Mataifa zinazotekelezwa nchini Tanzania walipozuru katika ofisi hizo kwa mazungumzo.

“Kuna ongezeko kubwa la ufahamu kuhusu haki za binadamu, upatikanaji wa haki kwa makundi maalumu, uandishi wa habari kuhusu haki za binadamu na kuboreshwa kwa huduma za kisheria na ukaribu wa serikali wa kufanyakazi na wadau wa haki za binadamu,” alisema Massay akifafanua zaidi kuhusu manufaa ya ufadhili wa Umoja wa Mataifa katika kuboresha haki za binadamu nchini.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga (wa pili kushoto) akitoa neno la ukaribisho kwa wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa (hawapo pichani) ulipotembelea tume hiyo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto), Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay (wa pili kulia), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Awa Dabo (kulia).(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Katika mazungumzo yao na ujumbe wa nchi za Nordic ambazo ni Sweden, Denmark, Norway Finland na Iceland kulikuwepo pia asasi mbalimbali zisizo za kiserikali kama Women’s Legal Aid Center, Tanzania Women Lawyers Association, Tanzania Women Judges Association, Legal Aid and Human Rights Center, Human Rights Defenders Coalition, na Tanganyika Law Society.

Katika mazungumzo hayo asasi hizo zilielezea ufanyaji kazi wao mafanikio na changamoto wanazokumbana nazo na umuhimu wa ufadhili wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Akizungumzia changamoto zinazokabili Umoja wa Mataifa, serikali na asasi Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez alisema ipo haja ya kuwa na muono wa muda mrefu wa kuratibu shughuli zinazohusiana na maendeleo endelevu.

Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay akizungumzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na tume hiyo kwa ujumbe kutoka nchi za Nordic ulioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa (hawapo pichani) ulipotembelea tume hiyo.

Alisema kwamba mabadiliko ya kitabia kwa binadamu huchukua muda mrefu kukubalika hivyo ni wajibu wa kila mmoja kufanya bidii ya kuhakikisha kwamba maisha yanabadilika na watu wanakumbatia mambo ya kisasa yanayochochea maendeleo yao na jamii

Akizungumza kwa niaba ya wajumbe kutoka nchi hizo za Nordic, Anders Rönquist, ambaye ni kiongozi wa ushirikiano wa kimataifa wa Shirika la Misaada la Sweden (SIDA), alisema pamoja na changamoto zilizopo kitaasisi, kisiasa, kifedha na kitamaduni maendeleo yaliyopo katika sheria na haki za binadamu nchini Tanzania yanatia moyo sana.

Alisema ipo haja ya serikali kuendelea kuhimiza mabadiliko na kwamba wao wapo tayari kusaidia mkakati wa kuboresha masuala ya sheria na haki za binadamu.

Kiongozi wa ushirikiano wa kimataifa wa Shirika la Misaada la Sweden (SIDA), Anders Rönquist (kulia) akizungumza kwa niaba ya wajumbe kutoka nchi hizo za Nordic ulipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Awa Dabo (kulia), akizungumza katika mkutano huo ambapo alishukuru mataifa hayo kwa kuendelea kusaidia programu za haki a binadamu nchini Tanzania. Alisema kwamba haki za binadamu ni kitu cha msingi katika maendeleo kwa kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila kuwapo na haki za binadamu. Alisema kwamba maendeleo na haki za binadamu ni mambo yanayoshabihiana na kuimarika kwake kunasaidia kuimarisha ustawi wa jamii. Alishukuru pia serikali ya Tanzania kwa kuhakikisha kwamna masuala ya utawala bora na haki za binadamu yamo katika mpango wa miaka mitano wa maendeleo ambao unasaidiwa pia na UNDAP ll.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga akisisitiza jambo kwenye mkutano na wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto (WLAC), Theodosia Muhulo akielezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo chake katika kuhakikishwa wanawake na watoto wapata msaada wa kisheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mwansheria kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Benedict Ishabakaki akizungumzia shughuli mbalimbali wanazofanya za msaada wa kisheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti wa TAWLA, Sophia Wambura aki-'share' uzoefu wake katika masuala ya sheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa neno la shukrani kwa Mwenyekiti wa THBUB wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti wa TAWLA, Sophia Wambura akikabidhi zawadi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) baada ya kumalizika mkutano wa wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Eusebia Munuo akikabidhi zawadi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipokutana na uongozi wa ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB).


 

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.

No comments: