Friday, November 4, 2016

TBS WATOA ZAWADI KWA WAANDISHI BORA WA INSHA ZA MAZINGIRA KWA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
SHIRIKA la Viwango Nchini (TBS) limewatangaza washindi wa shindano la uandikaji wa insha lililoandaliwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) lililoshirikisha shule za msingi na sekondari Tanzania nzima.

Akizungumza kabla ya utoaji tuzo hizo,Kaimu mkurugenzi mkuu wa TBS Egid Mubofu amesema hatua hii itasaidia sana kuweza kutoa elimu kwa wananchi hasa baada ya wanafunzi hawa kuonesha jitihada kubwa za kuondokana na suala zima la uchafuzi wa mazingira.



Katika shindano hilo lililoshirikisha takribani wanafunzi 75 kutoka sehemu mbalimbali nchini lilianza rasmi mwezi Septemba na kumalizika mwishoni mwa mwezi Oktoba na kufanikiwa kupatikana kwa washiriki nane kwa shule za Msingi na 10 kutoka shule za Sekondari.



Mshindi wa kwanza kwa upande wa shule ya msingi ilichukuliwa na Nairath Ngururu kutoka shule ya Wasichana Almutanzir huku nafasi ya pili ikiendelea Eldred Medard kutoka shule ya Valentine na nafasi ya tatu kwenda kwa Shiluni Laizer kutoka shule ya Havard zote za Jijini Dar es salaam.

kwa upande wa sekondari,wasichana waliendelea kutamba baada ya Zainab Kambi kutoka Academic Internaational kushika nafasi ya kwanza, Frank Kapinga kutoka Kibaha Sekondari kushika nafasi ya pili na nafasi ya tau kuchukuliwa na Pius Mollel kutoka St Jude
 ya Jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa mradi huo, Mary Meela amesema kuwa washiriki wote ni washindi kwani waliweza kuingia kwenye hatua ya mwisho ya mchujo na wanatakiwa kuja kuwa mabalozi wakubwa katika suala zima la mazingira.

Afisa mwakilishi wa UNEP, Clara Nakenya amesema kuwa hatua hii ni moja ya malengo 12 yaliyofikiwa kwa ajili ya kupambana na masuala ya mazingira kwani insha hizi zina elimu ya kutosha kwa rika zote husuani watoto, vijana na wazee katika kufanya maamuzi kuhusiana na mazingira.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa TBS Egid Mubofu akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa shindano hilo walioingia fainali pamoja na majaji wa shindano hilo.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) Egid Mubofu akizungumza wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano uandishi wa insha wa mazingira lililoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika hilo.
Afisa mwakilishi wa Shirika la Mazingira Duniani (UNEP), Clara Nakenya akizungumza wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano uandishi wa insha wa mazingira lililoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika hilo.
Jaji mkuu wa shindano hilo, Jumanne Mpinga akitolea ufafanuzi namna washiriki walivyoonyesha juhudi kubwa kwa kuandika insha nzuri zenye kuleta elimu kwa jamii kuhusiana na mazingira.
Mshindi wa kwanza kwa upande wa shule ya Msingi Nairath Ngururu kutoka shule ya Wasichana Almutanzir(kushoto) na Mshindi wa kwanza upande wa shule ya sekondari Zainab Kambi kutoka Academic Internationa wakiwa katika picha ya pamoja na Kaimu mkurugenzi wa Shirika la Vwiango Nchini (TBS) Egid Mubofu pamoja na Afisa mwakilishi wa Shirika la Mazingira Duniani (UNEP), Clara Nakenya.
Mwenyekiti wa mradi , Mary Meela akizungumza wakati wa utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano uandishi wa insha wa mazingira lililoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika la Viwango Nchini TBS.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) Egid Mubofu akimkabdhi cheti cha heshima kwa jaji mkuu wa shindano hilo wakati wa iutoaji zawadi kwa washindi na washiriki wengine.





Kaimu mkurugenzi mkuu wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) Egid Mubofu akikabidhi vyeti kwa washiriki mbalimbali wa Shindano la uandishi wa Insha inayihusiana na mazingira iliyoratibiwa na Shirika la Mazingira Duniani (UNEP) kushirikiana na shirika LA viwango nchini TBS.
Wazazi na washiriki wa Shindano wakiwa makini kusikiliza kabla ya utoaji wa zawadi.

No comments: