Tuesday, October 25, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHUTUBIA KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA MIAKA 55 YA UDSM

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongozana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandala (kulia kwake) kuelekea kwenye ukumbi wa Nkurumah baada ya kuwasili kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuhutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo hicho Oktoba 25, 2016. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ally Happy, kushoto ni Rais wa Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jaji Joseph Warioba na wapili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinoloji, Dkt. Leonard Akwilapo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa na makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandala baada ya kwasili kwenye ukumbi wa Nkurumah chuoni hapo kuhutubia kwenye kilelele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo hicho Oktoba 25, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akihutubia kwenye kilele cha Maadhiisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.
Baadhi ya waliohudhuria kwenye kilele cha Maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipowahutubia kwenye ukmbi wa Nkuruma jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Kitabu Kiitwacho From Lumumba Street to the Hill and Beyond katika kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaa baada ya kuhutubia kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016. Katikati ni Makamu Mkuu wa CHuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandala na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Dkt Leonard Akwilapo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha Kitabu Kiitwacho From Lumumba Street to the Hill and Beyond baada ya kukizindua katika kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es salaa baada ya kuhutubia kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam. Katikati ni Makamu Mkuu wa CHuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukanda na kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Dkt Leonard Akwilapo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Rais wa Jumuiya wa Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Jaji Joseph Warioba baada ya kuhutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya chuo hicho kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam wa zamani, Balozi Nicholas Kuhanga baada ya kuhutubia kwenye Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo hicho kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dae es salaam wa zamani Profesa Matthew Luhanga baada ya kuhutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya Miaka 55 ya Chuo hicho kwenye ukumbi wa Nkurumah jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: