Tuesday, October 25, 2016

MAENDELEO BENKI YAFUNGUA TAWI JIPYA

Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Benki Bw. Ibrahim Mwangalaba akizungumza na wageni waalikwa jana katika uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo lililopo Mwenge jijini Dar es Salaam,kulia kwake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Benki Bw. Amulike Ngeliama na Mjumbe wa Bodi hiyo Bw. Naftal Nsemwa.
Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Benki Bw. Ibrahim Mwangalaba akiwaongoza wageni waalikwa katika maeneo mbalimbali ya tawi jipya la Mwenge, Dar es Salaam lililozinduliwa jana.
Wageni waalikwa katika hafla fupi ya ufunguzi wa tawi jipya la Maendeleo Benki la Mwenge wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa tawi hilo mapema jana
Baadhi ya wateja wakipata huduma za kibenki katika tawi la Maendeleo Benki lililofunguliwa leo jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Maendeleo Benki Bw. Amulike Ngeliama akipata huduma katika tawi jipya la benki hiyo baada ya uzinduzi Mwenge, Dar es Salaam

No comments: