Friday, October 28, 2016

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA ATEMBELEA MRADI WA UZALISHAJI KOKOTO WA SUMA - JKT, PONGWE MSUNGULA MKOANI PWANI

Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja akisalimiana na baadhi ya Maafisa Watendaji katika mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula, Mkoa wa Pwani leo Oktoba 28, 2016 alipotembelea mradi huo ili kujionea shughuli za uzalishaji wa kokoto.
Meneja Msaidizi wa Mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula, Kepteni Gaspa Rugayana akitoa maelezo mafupi kuhusiana na mradi huo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kulia).
Ujumbe wa Maafisa Watendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza(Prisons Corporation Sole) ambao umefuatana na Kamishna Jenerali wa Magereza katika ziara ya mafunzo kwenye mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula, Mkoa wa Pwani. Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza linatarajia kuanzisha mradi wa Uzalishaji kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.
Maafisa Watendaji wa SUMA – JKT katika mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula wakimtembeza katika maeneo mbalimbali Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(wa tatu kulia) alipofanya ziara ya mafunzo katika mradi huo(kulia) ni Meneja Fedha na Utawala katika Mradi huo, Bi. Glory Kimaro.
Meneja Uzalishaji wa mradi wa kokoto, Kepteni Paul Mbeya akimuonesha mtambo wa uzalishaji kokoto Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kulia).
Mtambo wa Uzalishaji katika mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Msungula kama unavyoonekana katika picha. Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza linatarajia kuanzisha mradi wa Uzalishaji kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.
Meneja Mkuu wa Mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT, Bw. Semih Yaran akimuonesha Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(wa pili kulia) maeneo mbalimbali ya mradi huo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP- John Casmir Minja(kulia) akiangalia kokoto za kutengenezea barabara zinazozalishwa katika mradi huo. Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza linatarajia kuanzisha mradi wa Uzalishaji kokoto katika eneo la Gereza Msalato, Mkoani Dodoma.
Muonekano wa kokoto zinazozalishwa katika Mradi wa Uzalishaji kokoto wa SUMA – JKT uliopo Pongwe Musungula(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

No comments: