Saturday, October 15, 2016

BENKI YA POSTA TANZANIA (TPB) YAMALIZA TATIZO LA UHABA WA VYOO KWA WALIMU WA SHULE YA MSINGI IPINDA KYELA

Meneja Mahusiano kwa Umma benki ya Posta Tanzania (TPB) Noves Moses akizungumza katika hafla ya Makabidhiano ya mradi wa vyoo vya walimu vyenye matundu matano katika shule ya Msingi Ipinda Wilayani Kyela Mkoani Mbeya ambavyo ujenzi wake umeghalimu kiasi cha shilingi milioni 8kwa msaada wa benki hiyo ya Posta Tanzania. 
Baadhi ya wananchi,walimu na wazazi pamoja na wanafunzi shule ya Msingi Ipinda Wilayani Kyela Mkoani Mbeya waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya vyoo vya walimu vilivyo jengwa kwa msaada wa benki ya Posta Tanzania TPB. 
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ipinda Wilayani kyela Mkoani Mbeya wakitoa burudani katika hafla ya makabidhiano ya vyoo vya walimu vyenye matundu matano ambavyo vimejengwa kwa msaada wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) kwa thamani ya shilingi milioni 8. 
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Ipinda Subira Gwakabale akishukuru kwa kupatiwa msaada na benki ya Posta Tanzania (TPB) kwa kujengewa vyoo vya walimu vyenye matundu 5 kwa thamani ya shilingi milioni 8 ,ambapo pia katika katika shukrani zake ameelezea changamoto mbalimbali walizonazo ikiwa ni pamoja na Idadi kubwa ya wananfunzi kuliko vyumba vya madarasa walivyo navyo ambapo kwa sasa wana jumla ya wanafunzi 948 huku vyumba vya vya madarasa vikiwa 8 tu hali ambayo inawawia vigumu katika utoaji wa huduma kwa wanafunzi hao. 
Meneja wa Benki ya Posta Tanzania Tawi la Mbeya ,Humphrey Julias akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano ya vyoo vya walimu vyenye matundu matano ambavyo vimejengwa na benki hiyo katika shule ya Msingi Ipinda Wilayani Kyela.
Afisa Taaluma Wilaya ya Kyela Lucasian Kavishe akiwaasa wananchi waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya vyoo vya walimu vilivyojengwa katika Shule ya Msingi Ipinda kwa Msaada wa Benki ya Posta Tanzania (TPB)kwa kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa wadau mbalimbali wanaojitolea katika miradi mbalimbali ya kusaidia sekta ya elimu ili kuendelea kuwapa moyo zaidi wa kusaidia 
Meneja wa benki ya Posta Tanzania (TPB)Mkoa wa Mbeya kulia ,Humphrey Julias akiteta jambo na Meneja Mahusiano kwa Umma wa benki hiyo Noves Moses kabla ya kukabidhi rasmi mradi wa vyoo vya walimu vyenye matundu matano vilivyojengwa katika shule ya Msingi Ipinda Wilayani Kyela Mkoani Mbeya kwa Msaada wa benki hiyo kwa thamani ya shilingi milioni 8. 
Meneja Mahusiano kwa Umma wa benki ya Posta Tanzania TPB,Noves Moses akizindua na kukabidhi rasmi mradi wa vyoo vya walimu vyenye matundu Matano ujenzi ambao umeghalimu kiasi cha shilingi milioni8 katika shule ya Msingi Ipinda Wilayani kyela Mkoani Mbeya Otobar 13 mwaka huu,kushoto ni mwenyekiti wa kijiji cha Ipinda Saadat Sam (katikati)Afisa elimu taaluma Lucasian Kavishe na mwalimu Mkuu wa shule hiyo Subira Gwakabale kulia . 
Muonekano wa jengo la vyoo vya walimu katika shule ya Msingi Ipinda lenye matundu matano ambalo ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi milioni8. 

Meza kuu katika Picha ya pamoja na walimu na wajumbe wa bodi ya shule ya Msingi Pinda.
Meza kuu na wafanyakazi wa benki ya Posta Tanzania TPB tawi la Kyela na Mbeya. 
Meza kuu katika picha ya pamoja na wadau na viongozi wa serikali ya kijiji cha Ipinda Wilaya ya Kyela. 
Vyoo vilivyokuwa vikitumiwa na walimu wa shule ya Msingi Ipinda kabla ya kujengewa vyoo vipya na benki ya Posta Tanzania (TPB).PICHA E.MADAFA 

No comments: