Wednesday, September 7, 2016

Bunge lapitisha muswada wa sheria ya upatikanaji wa taarifa ya mwaka 2016




Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa Michezo akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016 ambapo alisema Muswada huu utasaidia kuongeza uwazi na uwajibikaji pia utasaidia kukuza tasnia ya habari nchini, Wakati wa Kikao cha 2 leo Bungeni Mjini Dodoma.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Watu wenye Ulemavu) akichangia akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016 ambapo alisema Muswada huu utasaidia kukidhi hitaji la kikatiba la watu kupata taarifa, Wakati wa Kikao cha 2 leo Bungeni Mjini Dodoma.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Masaju akichangia hoja kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016 ambapo alisema na kusisitiza umuhimu wa muswada huu ikiwemo kuongeza wigo wa upatikanaji wa taarifa kwa waandishi wa habari.



Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe akijibu hoja zilizotolewa na wabunge kuhusu Muswada wa Sheria ya upatikanaji wa Taarifa ya mwaka 2016 ambapo aliwataka wabunge kuacha kupotosha kuwa muswada huu utavibana vyombo vya habari na kuwataka kuusoma na kuuelewa muswada huo. PICHA NA HASSAN SILAYO
Eleuteri Mangi na Batrice Lyimo-Dodoma


Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Taarifa wa mwaka 2016 ili ufuate hatua ya kusainiwa na Rais akiwa sehemu ya Bunge ili uweze kuwa sheria kamili itkayotumika Tanzania Bara.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya kamati ya Bunge zima kumaliza kazi yake saa 2:15 usiku ya kupitia kifungu kwa kifungu na kukubali pamoja na marekebisho yake.
Awali kwa upande wa Serikali wakijibu hoja za Wabunge kuhusu Muswada huo walisema utasaidia kupanua wigo wa upatikanaji wa taarifa, utasaidia kukuza tasnia ya habari, utakidhi hitaji la Kikatiba la watu kupata taarifa.
Upande wa Serikali uliwakilishwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Harrison Mwakyembe, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Gerge Masaju, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi Waziri Mkuu (Watu Wenye Ulemavu)  Dkt. Abdallah Possi



Kupitishwa kwa Muswada huo ni kutekeleza matakwa ya kifungu cha Sheria cha 18 cha Katiba ya nchi ambacho kinatoa haki ya mtu kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali ya nchi na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha ya shughuli za maisha ya wananchi na masuala ya kijamii.
Aidha, Muswada huo utasaidia upatikanaji wa taarifa ambazo ni nyenzo muhimu na chachu ya maendeleo ya taifa.
Muswada uliopitishwa leo na Bunge mjini Dodoma umejadiliwa kwa muda wa siku mbili ambapo jumla ya Wabunge 44 wamechangia hoja wakati wa mjadala, Wabunge 39 wametoa michango yao kwa njia ya kuongea wakati wa Bunge na Wabunge watano wamechangia hoja zao kwa maandishi.

No comments: