Wednesday, July 6, 2016

WANANCHI WAFURIKA BANDA LA PPF MAONESHO YA BIASHARA YA KIMATAIFA SABASABA

Mkurugenzi wa Majanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Uphoo Swai, akimkabidhi Kitambulisho Clara Benard, mmoja kati ya wanachama wapya waliojiunga na Mfuko wa PPF kupitia huduma ya Wote Scheme, katika Banda la PPF kwenye Maonesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Picha na Mafoto Blog
Meneja Uhusiano Lulu Mengele na Meneja Masoko Elihuruma Ngowi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, wakiwahudumia baadhi ya wanachama waliojiunga na huduma ya Wote Scheme, katika Banda la PPF.
Mkurugenzi wa Majanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Uphoo Swai, akimkabidhi Kitambulisho Mwita Bony, mwanachama mpya aliyejiunga na Mfuko wa PPF.
Afisa Uendeshaji wa Kanda ya Temeke, Sosteness Lyimo, akiwahudumia baadhi ya wananchi waliotembelea Banda la PPF leo.
Mkurugenzi wa Majanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Uphoo Swai, akimkabidhi Kitambulisho Mtani Manoko, mwanachama mpya aliyejiunga na Mfuko wa PPF.
Mkurugenzi wa ukaguzi wa ndani wa PPF, Bw. Hosea Kashimba (kushoto) na Mkurugenzi wa Majanga, Uphoo Swai (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wapya waliojiunga na Mfuko wa PPF leo.
Maafisa wa Mfuko wa PPF, Mwajuma Msina na Pauline Msanga, wakiwahudumia wateja waliotembelea kwenye Banda hilo, leo.
Maafisa wa Mfuko wa PPF, wakiwahudumia wateja waliofika kujua michango yao.
Mkurugenzi wa Majanga wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Uphoo Swai, akimkabidhi Kitambulisho Filipa Sylvester, mwanachama mpya aliyejiunga na Mfuko wa PPF.
Mkurugenzi wa ukaguzi wa ndani wa PPF, Bw. Hosea Kashimba (wa saba kutoka kulia) na Mkurugenzi wa Majanga, Uphoo Swai (wa saba kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko wa PPF wakiwa na Tuzo yao waliyokabidhiwa kwenye Maonesho ya Biashara ya Kimataifa.

No comments: