Monday, July 4, 2016

USIKU WA RICHARD GWAPULUKWA WA GEITA ALIPOUKACHA UKAPELA.

Baada ya Kufunga ndoa jana June 03,2016 katika Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba Manispaa ya Ilemela Jijini Mwanza, Bibi harusi Happness Daniel Kulola wa Jijini Mwanza (kushoto) pamoja na mmewe Richard Jeremiah Gwapulukwa wa Kasamwa mkoani Geita, wamefurahia usiku wao katika Sherehe iliyofanyika kwenye ukumbi wa New Sun City Hotel Jijini Mwanza kuamkia leo. Pichani ni maharusi wakikata keki ukumbini. NaPicha zote na BMG
Bwana harusi akiwakabidhi keki wazazi wake upande wa bibi harusi
Bibi harusi akiwakabidhi keki wazazi wake upande wa bwana harusi
Maharusi wakiwa ukumbini. Wa kwanza kushoto ni Patron na wa kwanza kulia ni Matron
Maharusi wakiwa Ukumbini. Kumbuka bibi harusi ni binti wa mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola.
Mshereheshaji katika ubora wake kwenye kufungua shampeini
Maharusi wakinyweshana shampeni.
Bibi harusi akiwa katika picha ya pamoja na wazazi wake
Maharusi wakiwakaribisha ndugu, jamaa na marafiki kupata chakula
Taswira ya Ukumbini

No comments: