Friday, July 29, 2016

IDARA ZA UHAMIAJI TANZANIA NA ZAMBIA ZAKUTANA DAR ES ES SALAAM LEO.

Na Chalila Kibuda, Globu  Jamii.
IDARA ya Uhamiaji nchini imekutana na Idara ya Uhamiaji ya nchini Zambia kujadili masuala ya uhamiaji kati nchi mbili juu wananchi katika nchi hizo kufuata taratibu za uhamiaji.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Naibu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji na Msemaji wa Idara hiyo, Abbas Irovya amesema  kuwa kuna watanzania walikamatwa nchini Zambia 4000 ambao walikuwa wanajishughulisha na ususi.

Irovya amesema kuwa kuna watu wanaghushi hati ya kusafiria na kudai kuwa wanataiboresha ili wasiweze kughushi hati hizo na wataobanika kuwa na hati hizo watachukuliwa hatua katika vyombo dola.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji wa Zambia, Moola Milomo amesema kuwa kuna fursa za ususi nchini humo na kutaka watanzania kufuata utaratibu wa idara ya uhamiaji.

Amesema kuna changamoto kwa watu wanaoingia nchini Zambia lakini Tanzania na inakabiliwa nazo hivyo kunahitaji utatuzi.
  Naibu Kamishna wa Idara Uhamiaji, Abbas Irovya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na maswala mbalimbali yanayojitokeza kwenidara hiyo kati ya Tanzania na Zambia.
Naibu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji, Abbas Irovya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji nchini Zambia, Moola Milomo.
Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji nchini Zambia, Moola Milomo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kumaliza mkutano wa kujadili masula ya uhamiaji kati ya nchi Zambia na Tanzania. Kushoto ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Abbas Irovya.





Baadhi ya Watendaji mbalimbali Idara ya Uhamiaji wa Tanzania na Zambia wakiwa katika mkutano wa kujadili masuala ya uhamiaji kati ya nchi ya Tanzania na Zambia katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

No comments: